Tuwasaidie Majirani Zetu Kutambua Thamani Ya Biblia
1 Yesu alitoa kwa wanafunzi wake yale waliyohitaji. Tunasoma katika Luka 24:45: “Ndipo akafungua kabisa akili zao ili kuifahamu maana ya Maandiko.” Alijua kwamba ili wapate ukubali wa Baba yake, wangepaswa kujifunza na kuelewa Neno la Mungu, Biblia. (Zab. 1:1, 2) Mahubiri yetu yana kusudi lilelile. Tunataka kuanzisha mafunzo ya Biblia ili ‘kufundisha watu kushika yote ambayo Yesu aliamuru.’ (Mt. 28:20) Tulindapo hilo akilini, tuchunguze madokezo fulani fulani yanayoweza kuwa ya lazima wakati wa ziara za kurudia.
2 Ikiwa mazungumzo yetu ya kwanza yalitegemea kitabu “Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?,” tunaweza kurudilia hivi:
◼ “Ningependa kuzungumza nawe juu ya nukta nyingine inayoonyesha thamani yenye kutenda kazi ya mashauri ya Biblia. Watu wengi wanaona kwamba ni vigumu kuelewana na wengine. Nini tunaweza kufanya ili kutengeneza uhusiano wetu pamoja na ujirani wetu? [Tusikilize jibu, tufungue kitabu kwenye ukurasa 168 fungu la 15, na tusome Mathayo 7:12. Tuongeze mawazo ya fungu la 16.] Ni kielelezo kingine cha hekima tunachopata katika mashauri ya Biblia. Nitakaporudi, ningependa kukuonyesha mashauri ambayo Biblia inatoa kwa ajili ya maisha ya familia yenye furaha.” Tuagane siku ili kurudi tena kuzungumzia kurasa 170-2, ambapo tunakuta mashauri ya Biblia kwa ajili ya maisha ya familia yenye furaha.
3 Ikiwa mtu alionyesha kupendezwa kwa ajili ya Biblia, tunaweza labda kuanzisha funzo la Biblia kama ifuatavyo:
◼ “Watu wote au karibu wote wangependa kuishi katika ulimwengu wenye amani na ulio hakika. Kwa kuwa ni tamaa ya wote, kwa nini kuna machafuko mengi na jeuri ulimwenguni? [Tusikilize jibu.] Biblia Traduction du monde nouveau inakuonyesha wapi utapata jibu kwa ulizo hilo katika Biblia.” Tuifungue kwenye ukurasa 1655 na tuonyesha shemu “Sujets de conversation bibliques”, Na. 23a: “Auteur de la détresse mondiale.” Tusome 2 Wakorinto 4:4. Tufasirie kwamba Mungu atamharibu Shetani na atasimamisha ulimwengu wenye amani na furaha yenye kudumu. Tusome Ufunuo 21:3, 4. Tunaweza kusema baadaye: “Wakati nitakaporudi, ningependa kukuonyesha maandiko fulani yanayofasiria kwa nini unaweza kutumaini katika ulimwengu usio na taabu.”
4 Ikiwa ufundi wa kuanzisha funzo moja kwa moja umetoa matokeo mazuri, tunaporudi nyumbani kwa mtu tunaweza kusema:
◼ “Mara ya mwisho tulitaja sababu fulani fulani kwa ajili ya hizo ni lazima kujifunza Biblia. Yeye anayetaka kujitaabisha kwelikweli anaweza kupata furaha ya kuvumbua yale Mungu anatuahidi. [Tusome Yohana 17:3.] Programu yetu ya mafundisho ya Biblia imekwisha kuwasaidia maelfu ya watu kujifunza mengi zaidi juu ya yale Mungu alituahidi na juu ya namna sisi tunaweza kumfurahisha.” Tuchukue kitabu Ujuzi, tuchunguze kichwa cha sura mbalimbali na tuonyeshe jinsi funzo la Biblia linavyoendeshwa.
5 Kwa kuwasaidia watu wanyofu kutambua thamani ya ajabu ya Neno la Mungu, tunawatolea msaada bora kuliko. Hekima wanayoweza kupata kwa kujifunza yenyewe inaweza kuwa “mti wa uzima” na kuwapa furaha kubwa.—Mit. 3:18.