Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 4/97 uku. 1
  • ‘Tujenge Watu Wa Nyumbani Mwetu’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Tujenge Watu Wa Nyumbani Mwetu’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Tuwajulishe Wengine Siri Ya Kupata Furaha Ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Tusaidie Familia Kujijengea Wakati Ujao Udumuo
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Toleeni Watu wa Umri Zote Kitabu Furaha ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Tutajifunza Kitabu Furaha Ya Familia
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 4/97 uku. 1

‘Tujenge Watu Wa Nyumbani Mwetu’

1 Hakuna shaka kwamba, popote ulimwenguni, maisha ya familia yanaharibika. Ulimwengu unaotawaliwa na Shetani unafurahia uongo na ufisadi. (1 Yn. 5:19) Hilo linakazia kwamba ni jambo la lazima zaidi kuliko sisi ‘kuwajenga watu wa nyumbani mwetu’ na kufundisha watu wengine jinsi wanavyoweza kujenga watu wao wa nyumbani.​—Mez. 24:​3, 27.

2 Kanuni za Biblia ni Ulinzi: Matumizi ya kanuni za Biblia ni ufunguo wa furaha halisi ya familia. Kweli zenye nguvu za Biblia ni zenye faida kwa kila mshiriki wa nyumbani katika hali zote za maisha. Kwa kuzitumikisha, familia ni yenye furaha na inakuwa na amani ya kimungu. ​—Ona Isaya 32:​17, 18.

3 Kanuni zinazotuwezesha kujenga watu wa nyumbani mwetu zinaonyeshwa wazi kwa urahisi katika kitabu kipya Siri ya Kupata Furaha ya Familia. Kila sura inamalizika na kisanduku kinachokazia kanuni ambazo washiriki wa familia wanapaswa kukumbuka. Vingi vya visanduku hivyo vinaanza na ulizo “Kanuni Hizi za Biblia Zaweza Kusaidiaje. . . ?” Hilo linavutia uangalifu wetu juu ya wazo la Mungu, likikazia ndani yetu maoni yake juu ya habari inayozungumziwa.​—Is. 48:17.

4 Tufahamiane na kitabu hicho. Tujifunze kupata kanuni zinazoweza kutufaidi wakati kunapotokea magumu. Kitabu kinazungumzia maswali kama: kile inaomba kutafuta kwa mtu tunayetazamia kuoana naye (sura 2), msingi wa ndoa inayodumu na yenye furaha (sura 3), yale wazazi wanaweza kufanya ili kwamba watoto wao matineja wawe watu wazima wenye madaraka na wenye kumuogopa Mungu (sura 6), jinsi ya kulinda familia na uvutano mbalimbali wenye kuharibu (sura 8), kanuni zinazowezesha nyumba zilizo na mzazi mmoja kufanikiwa (sura 9), msaada wa kiroho kwa familia zilizo na magumu ya uzoevu wa alkoholi (vinywaji vikali vya kulevya) na jeuri ya kinyumbani (sura 12), jinsi ya kutenda wakati uhusiano wa ndoa unakaribia kuvunjika (sura 13), yale yanayoweza kufanywa ili kuwaheshimu wazazi wazee-wazee (sura 15) na jinsi ya mtu kujengea familia yake wakati ujao wa milele (sura 16).

5 Tutumie Kikamilifu Kitabu Kipya: Ikiwa hilo halijafanywa bado, kwa nini kutokujifunza katika familia kitabu Furaha ya Familia? Vivyo hivyo, ikiwa familia yetu inakutana na magumu mapya au inaishi hali yenye kusumbua, tuchunguze upya sura za kitabu zinazozungumzia magumu hayo na tufikiri katika sala jinsi ya kutumikisha mashauri hayo. Kwa upande mwingine, tuwe wakarimu kwa kupanga wakati ili kuhubiri na kujikaza kutolea kitabu Siri ya Kupata Furaha ya Familia kwa watu wengi zaidi iwezekanavyo mnamo mwezi wa Aprili.

6 Familia zinazoshikamana na ujitoaji-kimungu zitaimarika kiroho na zitakuwa zenye kuungana, tayari kuzuia mashambulio ya Shetani. (1 Tim. 4:​7, 8; 1 Pt. 5:​8, 9) Sisi ni wenye shukrani kama nini kwa Mwanzilishi wa familia anayetutolea mafundisho yake!

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine