Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Machi 15
“Je, unafikiri kwamba mafundisho ya Yesu ni yenye mafaa kwa wakati wetu? [Acha mtu ajibu.] Bila shaka utakubaliana na amri hii ambayo Yesu alitoa siku ya mwisho ya maisha yake. [Soma Yohana 15:12.] Yesu alifundisha pia mambo mengine ya thamani siku hiyo. Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linaonyesha jinsi tunavyoweza kufaidika kutokana nayo.”
Amkeni! Machi 22
“Je, umetambua kwamba ni vigumu kwa watu wengi leo kupata usingizi wa kutosha? [Acha mtu ajibu.] Hilo linaweza kusababishwa na mahangaiko au wasiwasi. [Soma Mhubiri 5:12.] Gazeti hili linazungumzia sababu fulani kati ya zile zinazosababisha kukosa usingizi, na linatoa madokezo yenye mafaa kuhusu jinsi tunavyoweza kuboresha tabia zetu za kusinzia.”
MNARA WA MLINZI Aprili 1
“Kinachoonyeshwa hapa ni kile kinachoitwa kwa kawaida Chakula cha Jioni. [Onyesha sehemu ya mbele na ya nyuma ya gazeti.] Je, ulijua kwamba hilo ndilo tukio moja tu ambalo Wakristo wanaamuriwa kukumbuka? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Luka 22:19.] Gazeti hili linaeleza kwa nini mwadhimisho huo ni wa lazima sana na uvutano ulio nao juu yako.”
Amkeni! Aprili 8
“Je, si jambo lenye kuhuzunisha kuona kwamba maisha ya vijana wengi yameharibiwa na dawa za kulevya? [Acha mtu ajibu.] Mara nyingi matatizo yanaanza vijana wanaposhirikiana na marafiki wabaya. [Soma 1 Wakorintho 15:33.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia jambo linalochochea vijana waanze kutumia dawa za kulevya na lile ambalo wazazi wanaweza kufanya ili kuwalinda.”