Kisanduku Cha Maulizo
◼ Je, ni jambo lenye kufaa kukusanya kutoka katika vitabu habari zitakazozungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi na kisha kuzigawia wengine?
Mnaruhusiwa kufanya hivyo ikiwa mtatumia habari hizo ninyi wenyewe au ikiwa mtazitolea washiriki wa familia zenu na marafiki zenu wa karibu. Hata hivyo, habari hizo hazipaswi kutolewa kwa watu wote au hamupaswi kuzitolea watu kwa kuwaomba feza, kwa kuwa kufanya hivyo ni kuvunja sheria inayohusu haki ya uchapishaji.—Rom. 13:1.
Kuhusu migawo fulani katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi, ni kichwa cha habari tu ndicho kinatolewa; hakuna kitabu chochote kinachoonyeshwa ili kusaidia kupata habari au maelezo. Je, lingekuwa jambo lenye faida mtu kutayarisha oroza ya mitajo au kukusanya habari kutoka katika vitabu, habari zinazoweza kutumiwa na wale wanaopewa migawo hiyo? Hapana. Pia si jambo linalofaa kukusanya kutoka katika vitabu majibu ya maulizo mbalimbali ya Kujikumbusha Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ili kuwagawanyia wengine kusudi yawasaidie kutoa majibu, kwa kuwa jambo hili halitawasaidia kuchunga akilini mambo makuu. Wanafunzi wanapaswa kutafuta majibu wao wenyewe katika vitabu. Hilo ni jambo la maana katika mazoezi ambayo Yehova anatutolea kupitia shule ili kutusaidia tuwe na “ulimi wa waliofundishwa.”—Isa. 50:4.