Jinsi ya Kutumia Kitabu “Upendo wa Mungu” Ili Kuongoza Mafunzo ya Biblia
1. Kitabu “Upendo wa Mungu” kina kusudi gani?
1 Kwenye Mkusanyiko wa Wilaya “Kuongozwa na Roho ya Mungu,” tulifurahi sana kupokea kitabu kipya “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”. Kama ilivyojulishwa, kitabu hicho hakikutayarishwa ili kutoa mafundisho ya msingi ya Biblia lakini kutusaidia kuelewa na kupenda kanuni za Yehova kuhusu mwenendo. Hatutatolea watu kitabu hicho katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba.
2. Namna gani kitabu hicho kitatumiwa, na kwa watu gani?
2 Kitabu hicho kitatumiwa kama kitabu cha pili cha kujifunza na wanafunzi wa Biblia kisha kumaliza kitabu Biblia Inafundisha. Kumbukeni kwamba watu hawafanye maendeleo ya kiroho kwa kadiri ileile. Kila funzo litaongozwa kulingana na uwezo wa mwanafunzi. Muwe hakika kwamba mwanafunzi anaelewa vizuri habari ambayo mulijifunza. Katika hali nyingi, kitabu hicho hakitatumiwa ili kuanzisha mafunzo ya Biblia na watu ambao labda wamekwisha kujifunza vitabu vingi nyakati zilizopita, lakini hawahuzurie mikutano ya kutaniko na kwa wazi hawapendi kutumia katika maisha yao kweli za Biblia ambazo wamejifunza.
3. Tutafanya nini ikiwa kwa sasa tunaongoza funzo katika kitabu Mwabudu Mungu?
3 Ikiwa kwa sasa unaongoza funzo katika kitabu Mwabudu Mungu na ikiwa munakaribia mwisho, unaweza kuamua kukimaliza na kumtia mwanafunzi moyo asome yeye mwenyewe kitabu “Upendo wa Mungu”. Ikiwa hamujakaribia mwisho, itakuwa vizuri zaidi kuhamishia funzo katika kitabu kipya na kuanzia mwanzoni. Kuzungumzia mambo yaliyo katika nyongeza ni uamuzi wa mutu mwenyewe, kama vile tunavyofanya kuhusiana na kitabu Biblia Inafundisha.
4. Tutafanya nini ikiwa mwanafunzi anabatizwa mbele ya kumaliza kujifunza kitabu Biblia Inafundisha na kitabu “Upendo wa Mungu”?
4 Ikiwa mwanafunzi anabatizwa mbele ya kumaliza vitabu vyote viwili, hivyo basi funzo litaendelea mpaka kumaliza kitabu “Upendo wa Mungu”. Hata ikiwa mwanafunzi amebatizwa, unaweza kuripoti saa, ziara ya kurudia na funzo la Biblia. Mhubiri anayekusindikiza na kushiriki pia katika funzo anaweza naye kuripoti saa.
5. Namna gani tunaweza kutumia kitabu “Upendo wa Mungu” ili kusaidia wahubiri ambao hawashiriki katika utumishi kwa muda fulani?
5 Ikiwa mshiriki fulani wa Halmashauri ya Utumishi ya Kutaniko anakutolea mgawo wa kujifunza na mutu fulani ambaye ameacha kutenda, labda utaombwa kuchunguza sura fulani za kitabu “Upendo wa Mungu”. Si lazima funzo kama hilo lichukue muda mrefu. Kitabu hicho kipya ni kifaa kizuri sana ambacho kimetayarishwa ili kutusaidia kuendelea “katika upendo wa Mungu”!—Yuda 21.