Ile Kazi ya Maana Zaidi
1. Kwa kuwa tunaona kazi ya kuhubiri kuwa ya maana zaidi, hilo linatuchochea kufanya nini?
1 Kwa nini kila mara tunatiwa moyo kutumia wakati wetu, nguvu, na mali yetu kwa ajili ya kazi ya kuhubiri? Kwa kuwa hakuna kazi ya maana zaidi kama kazi ya kuhubiri! Kufikiri sana juu ya matokeo makubwa yanayotokana na kazi hiyo kunatuchochea tuwe na nia zaidi ya kushiriki katika kazi hiyo ambayo haitarudiliwa tena.—Mdo. 20:24.
2. Namna gani kazi yetu ya kuhubiri inasaidia kutakasa jina kuu la Yehova?
2 Inatakasa Jina la Yehova: Kazi ya kuhubiri inakazia kwamba Ufalme wa Yehova unaotawaliwa na Kristo Yesu utachukua nafasi ya serikali za wanadamu na kumaliza matatizo yote ya wanadamu. (Mt. 6:9, 10) Yehova anatukuzwa kwa kuwa ni yeye tu aliye na uwezo wa kumaliza magonjwa na kifo. (Isa. 25:8; 33:24) Kwa kuwa tunaitwa kwa jina lake, wale wanaotazama mwenendo wetu safi na bidii yetu wanaweza pia kumtukuza. (1 Pet. 2:12) Ni jambo lenye kufurahisha kabisa kujulisha watu ulimwenguni pote jina la Yehova ambaye ni Mtawala Mkuu wa Ulimwengu Wote Mzima!—Zab. 83:18.
3. Wale wanaokubali ujumbe wa Ufalme wanapata baraka gani?
3 Inaokoa Uzima: Yehova “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” (2 Pet. 3:9) Hata hivyo, ikiwa hakuna mutu wa kuhubiri, namna gani watu watajifunza kujua mwenendo unaofaa na mwenendo usiofaa machoni pa Yehova? (Yona 4:11; Rom. 10:13-15) Wakati watu wanakubali habari njema, maisha yao yanakuwa mazuri zaidi wanapoacha mazoea yenye kuumiza. (Mik. 4:1-4) Pia, wanakuwa na tumaini la uzima wa milele. Kuhubiri na kufundisha kwa bidii kunatuokoa na kuokoa wale wanaotusikiliza. (1 Tim. 4:16) Sisi tuna daraka lenye kuheshimika kabisa katika kazi hiyo ya maana zaidi!
4. Kwa nini tuwe na mengi ya kufanya kadiri tuwezavyo katika kazi ya kuhubiri Ufalme na kufanya wanafunzi?
4 Hivi karibuni ziki kubwa italeta mwisho wa gafula kwa ulimwengu huu usio na haki. Wale watakaokuwa upande wa Yehova wataokoka. Kwa hiyo, kazi ya kuhubiri na kufanya wanafunzi tunayofanya leo ndiyo kazi ya maana na yenye faida inayoombwa kufanywa kwa haraka. Acheni basi tutie kazi hiyo pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu!—Mt. 6:33.