‘Jina la Mungu Litakaswe’
1. Mkusanyiko wa mzunguko wa mwaka wa utumishi wa 2012 una kichwa gani, na unategemea nini?
1 Tuna pendeleo kubwa la kuitwa kwa jina la Yehova, Mwenye Enzi Kuu! Ni Mungu mwenyewe aliyetupatia pendeleo hilo la kuitwa kwa jina lake, na hasa kuanzia mwaka wa 1931, tumejulikana kuwa Mashahidi wa Yehova na hivyo kutaja jina la pekee la Yehova kunamufanya mutu afikirie Mashahidi. (Isa. 43:10) Yesu, mwana-mzaliwa pekee wa Mungu, aliliheshimu sana jina la Mungu, alilitia pa nafasi ya kwanza katika sala aliyofundisha wanafunzi wake. (Mt. 6:9) Kichwa cha mkusanyiko wa mzunguko wa mwaka wa utumishi wa 2012 kinategemea maneno hayo ya Yesu. Kichwa cha mkusanyiko huo ni: ‘Jina la Mungu Litakaswe.’
2. Ni habari gani tunazongojea kwa hamu?
2 Mambo Tutakayosikia: Siku ya Posho tutasikiliza hotuba yenye kichwa: “Julisha Jina la Mungu kwa Kufanya Utumishi wa Wakati Wote.” Habari hiyo itaonyesha kwa nini utumishi wa wakati wote ndiyo njia ya maisha yenye kuleta baraka nyingi. Tutasikiliza pia hotuba-mfululizo yenye kichwa: “Fanya Angalisho ili Usilichafue Jina la Yehova.” Hotuba hiyo itatusaidia tusiangukie katika mitego ine. Hotuba yenye kichwa, “Kwa Nini Jina la Mungu Linapaswa Kutakaswa,” itajibu maulizo yafuatayo: Ni nini litakalotusaidia kuhubiri kwa bidii wakati watu wanaonekana kuwa hawapendezwi sana? na ni nini litakalotusaidia ili utumishi wetu uwe wenye matokeo mazuri? Siku ya Yenga tutakuwa na hotuba-mfululizo yenye sehemu ine zitakazozungumzia jinsi tunavyoweza kulitakasa jina la Mungu kupita mawazo yetu, maneno yetu, maamuzi yetu, na mwenendo wetu. Wapya watafurahia hasa hotuba ya watu wote, yenye kichwa “Yehova Atalitakasa Jina Lake Nzuri Kwenye Har-magedoni.”
3. Tuna pendeleo gani, na mkusanyiko wa mzunguko huu utatusaidia namna gani?
3 Hivi karibuni, Yehova atatenda ili kulitakasa jina lake. (Eze. 36:23) Lakini mbele ya jambo hilo kufanyika, tuna pendeleo kubwa sana la kutetea jina takatifu la Yehova kupitia maneno yetu na matendo yetu na kuepuka kufanya jambo lolote linaloweza kuchafua jina hilo. Tunatumaini kwamba mkusanyiko huu wa mzunguko utasaidia kila mmoja wetu kutimiza daraka lake kwa uzito; la kuwa mutu anayechukua jina la Mungu.