Kampanye ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho
1. Tutaanza kuwaalika watu kwenye Ukumbusho wakati gani, na sababu gani kampanye itachukua muda murefu mwaka huu?
1 Siku ya Tano, tarehe 1 Mwezi wa 3, tutaanza kampanye tunayofanya kila mwaka ili kuwaalika watu wahuzurie Ukumbusho pamoja nasi. Ukumbusho utafanywa tarehe 26 Mwezi wa 3, hilo linamaanisha kwamba kampanye itachukua muda murefu kuliko miaka iliyopita. Kwa hiyo, watu wengi zaidi watakuwa na nafasi ya kupata mialiko, zaidi sana ikiwa wanaishi mahali ambapo kutaniko lina eneo kubwa.
2. Ni mipango gani itakayofanywa ili kupata mialiko na kuitolea watu katika eneo?
2 Kupanga Mahubiri: Wazee watatoa muongozo wa kufuata kuhusu jinsi eneo litakavyohubiriwa, na pia ikiwa wahubiri wanaweza kuacha mialiko mahali ambapo hawakukuta watu. Baada ya eneo kuhubiriwa nyumba kwa nyumba, ikiwa mialiko inabaki, wahubiri wanaweza kuigawanya mahali pa watu wengi. Mwangalizi wa utumishi atahakikisha kwamba mialiko iliyo na maandishi yanayoonyesha mahali na saa ya ukumbusho imewekwa kwenye meza ya vitabu na magazeti ili wahubiri waichukue, lakini mialiko yote haitawekwa mara moja kwenye meza. Kila muhubiri anapaswa kuchukua tu mialiko atakayotumia katika juma moja.
3. Tunapaswa kukumbuka nini tunapomutolea mutu mualiko?
3 Yale Tutakayosema: Ni vizuri zaidi kusema mambo machache, hilo litatusaidia kuwatolea watu wengi mialiko, kadiri iwezekanavyo. Kwenye ukurasa wa 4 kuna namna ya kuanzisha mazungumuzo ambayo tunaweza kurekebisha ili ipatane na watu wa eneo letu. Kwa kweli, si lazima tuwe haraka ikiwa tunaona musikilizaji anapendezwa ao ana ulizo. Tunapotolea watu mialiko Siku ya Posho na Siku ya Yenga, ni lazima tuwatolee pia magazeti, inapofaa. Tarehe 2 Mwezi wa 3, tutatolea watu mialiko kuliko kuanzisha mafunzo ya Biblia.
4. Sababu gani tunapaswa kushiriki kwa bidii katika kampanye ya kuwatolea watu mialiko?
4 Tunatumaini kama watu wengi watahuzuria Ukumbusho pamoja nasi. Hotuba itaeleza Yesu ni nani kabisa. (1 Kor. 11:26) Itaonyesha namna gani kifo cha Yesu kinatufaidi. (Rom. 6:23) Pia, itatusaidia kuelewa sababu gani ni lazima tumukumbuke Yesu. (Yoh. 17:3) Acheni basi tushiriki kwa bidii katika kampanye hiyo!