Unaweza Kumualika Muhubiri Mwengine?
Katika makutaniko mengi, kuna wahubiri ambao wanahubiri kwa muda mufupi kwa sababu wana magonjwa yasiyopona ao kwa sababu wamezeeka. (2 Kor. 4:16) Unaweza kumualika muhubiri aliye katika hali kama hiyo ili ajiunge nawe unapoongoza funzo la Biblia? Ikiwa muhubiri huyo hawezi kutoka nyumbani, labda unaweza kuongoza funzo hilo nyumbani kwake. Je, unaweza mara kwa mara kumualika muhubiri ambaye ana matatizo ya afya ili uhubiri pamoja naye nyumba chache katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba ao kurudilia mutu mumoja ao watu wawili? Wahubiri wengi wenye kuzeeka wana ufundi mwingi katika mahubiri. Kwa hiyo, si wao tu ambao watafaidika kwa kutiwa moyo, wewe pia utafaidika na uzoefu wao. (Rom. 1:12) Zaidi ya hilo, Yehova atakulipa kwa kuwa unajikaza kuonyesha upendo kwa njia hiyo.—Met. 19:17; 1 Yoh 3:17, 18.