Kampanye ya Kuwatolea Watu Trakte Habari ya Ufalme Na. 38 Itafanywa Katika Mwezi wa 11!
1. Watu wanajiuliza ulizo gani kuhusu watu waliokufa, na namna gani ulizo hilo litajibiwa katika Mwezi wa 11?
1 Kifo ni adui ya kila mutu, iwe yuko katika dini gani. (1 Kor. 15:26) Watu wengi wanajiuliza ikiwa watu waliokufa wako wapi na ikiwa watapata kuwaona tena. Kwa hiyo, makutaniko ya duniani pote yatashiriki katika kampanye ya kuwatolea watu Trakte Habari ya Ufalme Na. 38. Trakte hiyo ina kichwa Watu Waliokufa, Wanaweza Kweli Kuishi Tena? Kampanye hiyo ya pekee itaanza tarehe 1 Mwezi wa 11. Kisha kampanye, trakte Habari ya Ufalme Na. 38 itatumiwa katika mahubiri kama trakte zingine.
2. Trakte Habari ya Ufalme Na. 38 imepangwa namna gani?
2 Namna Ambavyo Imepangwa: Trakte Habari ya Ufalme Na. 38 imepangwa ili ikunjwe kwa urefu hivi kwamba sehemu ya mbele ionyeshe kichwa cha trakte na maneno “Jibu lako ni . . . ndiyo? hapana? pengine?” Musomaji anapoifungua Trakte hiyo, ataona namna Biblia inavyojibu ulizo linalofanyiza kichwa cha trakte na faida atakayopata ikiwa anaamini fundisho hilo la Biblia. Pia, ataona sababu zinazoweza kumufanya aamini mafundisho ya Biblia. Sehemu ya nyuma ya trakte hiyo ina ulizo lenye kupendeza linalomufanya afikiri na hivyo ajifunze mengi zaidi.
3. Namna gani tutawatolea watu trakte Habari ya Ufalme Na. 38?
3 Namna Tutakavyoitolea Watu: Tutawatolea watu trakte Habari ya Ufalme Na. 38 kwa namna tunavyowatolea mialiko kwenye ukumbusho na kwenye mukusanyiko wa wilaya. Wazee watatoa muongozo kuhusu namna ya kuwatolea watu trakte hiyo katika eneo lote la kutaniko, kupatana na maagizo yaliyo katika barua ya tarehe 1 Mwezi wa 4, 2013. Ikiwa kutaniko lenu lina eneo ndogo, munaweza kusaidia kutaniko jirani lililo na eneo kubwa. Kutaniko lenu litakapopokea Trakte Habari ya Ufalme Na. 38, chukua tu zile ambazo unaweza kutolea watu muda wa juma. Wakati wa kampanye, kisha kutolea watu trakte nyumba kwa nyumba katika eneo lote, wahubiri wanaweza kuzitoa mahali pa watu wengi. Ikiwa trakte zote zinamalizika mbele kampanye ifikie mwisho, mutatolea watu vichapo vinavyopaswa kutolewa katika Mwezi wa 11. Siku ya Posho ya kwanza ya mwezi, tutatolea watu trakte Habari ya Ufalme Na. 38 kuliko kuanzisha mafunzo ya Biblia. Kila Siku ya Posho na ya Yenga, inapofaa, tutatolea watu magazeti. Unafanya mipango ili ushiriki kikamili katika kampanye hiyo ya pekee?