Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri—Kuandika Mambo Fulani Kuhusu Mutu Anayependezwa
‘Endelea kujiangalia wewe mwenyewe na kufundisha kwako.’ (1 Tim. 4:16) Hilo ni shauri lililoongozwa na roho ambalo mutume Paulo alimutolea Timoteo; linaonyesha kwamba tunapashwa kujikaza kufanya maendeleo, hata kama sisi ni wahubiri wapya ao wenye uzoefu. Ili kutusaidia, habari mupya yenye kichwa “Tukomalishe Ufundi Wetu wa Kuhubiri” itaanza kutokea katika Huduma Yetu ya Ufalme. Kila sehemu itazungumuzia ufundi fulani wa maana, na itatoa mapendekezo kuhusu namna ya kufanya. Sisi wote tunatiwa moyo kutumikisha ufundi huo katika mwezi. Mwezi unapomalizika, kwenye Mukutano wa Utumishi kutakuwa sehemu ambayo itatutolea nafasi ya kueleza namna tulifaidika kwa kutumikisha ufundi huo. Mwezi huu tunatiwa moyo kuandika mambo fulani kuhusu mutu anayependezwa.
Sababu Gani Ni Lazima Kufanya Hivyo: Ili kutimiza mugawo wetu, hatupashwe kuhubiri tu. Tunapashwa pia kuwarudilia wale waliopendezwa na kuwafundisha ili kumwangia maji mbegu za ukweli ambazo tulipanda. (Mt. 28:19, 20; 1 Kor. 3:6-9) Hilo linaomba tumutembelee tena mutu, tuzungumuzie mambo yanayomuhangaisha, na tuanzishe mazungumuzo kwa kufikiria mambo tuliyozungumuzia tulipoonana. Kwa hiyo, mutu akipendezwa, ni muzuri tuandike habari fulani juu yake.
Namna ya Kufanya:
• Hakikisha kwamba una vifaa vyote unavyoweza kutumia ili kuandika habari juu ya mutu anayependezwa. Andika habari waziwazi, uzipange muzuri, na zipatane na hali yake ya sasa. Fanya hivyo kisha tu kuachana na mutu.
• Andika habari kuhusu musikilizaji wako. Andika jina lake, adresi yake, namba yake ya telefone, ao adresi yake ya Internete. Ulitambua jambo gani la lazima kumuhusu yeye na familia yake ambalo unaweza kutumia ili kuendeleza mazungumuzo?
• Andika mambo muliyozungumuzia. Mulisoma maandiko gani? Alisema nini kuhusu mambo anayoamini? Ulimuachia vichapo gani? Andika siku, tarehe, na wakati.
• Andika mambo unayopanga kufanya wakati utarudi, habari muliyopanga kuzungumuzia, siku na wakati muliopanga kuonana tena.
• Kila mara unaporudi, andika habari za mupya kumuhusu. Haiko mubaya kuandika mambo mengi kumuhusu.
Tumikisha shauri Hili Katika Mwezi:
• Umuelezee yeyote unayehubiri naye mambo unayoandika.