Kila Andiko Lafaa Kwa Kufundisha
1 Maoni juu ya thamani ya Biblia ni mengi na yanatofautiana. Kwa upande wetu, tupo hakika kwamba kurasa zake zina majibu kwa magumu yenye kutatiza sana ya wanadamu, na pia mambo yenye kutumainika ili kutoa uongozi mzuri kwa maisha yetu. (Mit. 3:5, 6) Hakuna kinacholinganika na hekima ya mashauri ya Biblia. Hakuna kinachopita kanuni za adili ambazo inapendekeza. Ujumbe wayo ni wenye nguvu, kwa kuwa unaweza “kutambua mafikira na makusudio ya moyo.” (Ebr. 4:12, NW) Jinsi gani kuwasaidia majirani zetu kuelewa kwamba wanapaswa kuchukua kitabu hicho kinacholala kwenye rafu (étagère) na kuanza kukisoma kwa bidii? Tujaribu hivyo, mnamo Mei, madokezo yafuatayo yanayokusudiwa kwa kutolea Traduction du monde nouveau pamoja na kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu?
2 Tukijua kwamba hangaiko la wengi ni kutosheleza mahitaji yao ya msingi, tuanze nao mazungumzo hivi:
◼ “Watu wengi ambao ninakutana nao nyakati hizi wanasema kwamba hangaiko lao kubwa ni kutosheleza mapaswa yao ya kifedha. Wengi wananaswa katika pirikapirika za utafutaji wa vitu vya kimwili, jambo ambalo ni chanzo cha mikazo. Ni nini chanzo bora cha mashauri juu ya mambo hayo? [Tungoje jibu.] Nimeona kwamba Biblia inatoa mashauri yenye kutenda kazi yanayoweza kusaidia kuepuka magumu yasiyofaa. Tazama kielelezo kimoja.” Tufungue kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu kwenye ukurasa 163 na tusome 1 Timotheo 6:9, 10, linalotajwa kwenye fungu la 3. Tutoe mawazo mengine juu ya fungu la 4, kisha tutolee kitabu.
3 Tungeweza kufikiria dokezo lingine hili:
◼ “Tunaposoma gazeti au tusikiapo habari mbalimbali, tunasikia sikuzote jambo fulani lipya lenye kusikitisha, na wasiwasi wetu unaongezeka. [Tutaje tukio moja kutokana na habari yenye kuvuruga akili.] Jinsi gani kupambana na magumu ya namna hiyo? [Tungoje jibu.] Katika 1983, raisi wa Shirikisho ya Amerika (kwa wakati huo Ronald Reagan) alisema kwamba Biblia inayo ujumbe wa muhimu zaidi ambao haujapata kamwe kuandikwa na kwamba ‘katika kurasa zayo hupatikana jibu kwa matatizo yote ambayo mtu anaweza kukutana nayo.’ Maneno yake yanakumbusha yale ambayo Biblia yenyewe inasema. [Tusome 2 Timotheo 3:16, 17.] Ningependa kukuonyesha kwa nini tunaweza kuitumaini Biblia.” Tutokeze mawazo fulani mazito ya trakti Sababu kwa Nini Wewe Unaweza Kuitumaini Biblia. Tuombe kurudi ili kufasiria namna gani yenye kushangaza matukio tunayosikia sasa ulimwenguni yanatimiza unabii mbalimbali wa Biblia.
4 Ikiwa watu wengi wa eneo letu hawana dini, tujaribu namna hii ya kuanza mazungumzo:
◼ “Watu wengi hapa wanahisi kwamba vitabu fulani vitakatifu vinapingana na kwa hiyo vinakuwa tu ni hadisi za kuwazia. Wanaona mambo mengi mabaya yakifanywa kwa jina la dini hivi kwamba walipoteza tumaini hata katika Biblia. Kwanza, wanadamu wengi zaidi na zaidi wanajiuliza ikiwa Biblia ni Neno la Mungu au ni la binadamu. Wewe unafikiri nini?” Tungoje jibu. Kupatana na jibu hilo, tufungue kitabu Biblia—Neno la Mungu au la Binadamu? kwenye andiko linalozungumzia kizuia-mazungumzo au wazo la msikilizaji wetu, na tuzungumzie juu ya wazo moja au mawili. Kwa mfano, tungeweza kutumia mafungu 27 mpaka 29 yanayoanzia kwenye ukurasa 66 chini ya kichwa cha habari “Yesu—Mtu Halisi.”
5 Mfundishaji wetu mkuu anaangalia ili kwamba ujuzi wa mapenzi yake upatikane kwa yeyote anayependa kuupata. Mojawapo ya matendo mazuri zaidi tungeweza kufanya kwa faida ya majirani zetu ni kuwasaidia kuthamini kabisa Biblia; hilo linaweza kuokoa uhai wao.—Mit. 1:32, 33.