Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/96 uku. 3-4
  • “Wajumbe Wa Amani Ya Kimungu”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Wajumbe Wa Amani Ya Kimungu”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wale Watakaohudhuria Kwenye Kusanyiko Lingine
  • Ushirikiano Wenu ni wa Maana Sana
  • Julai 5-7 Kinshasa (F) KIN-4, KIN-7, KIN-10
  • Julai 19-21 Kinshasa (LI-2) KIN-2, KIN-5, KIN-6, KIN-9, KIN-11 Bukavu KI-1, KI-11, KI-12 Ilebo KA-10, KA-15, KA-21, KA-29 Mbuji-Mayi KA-2, KA-5, KA-13, KA-16, KA-17, KA-20, KA-25 Butembo KI-5, KI-7, KI-9, KI-10
  • Agosti 2-4 Brazzaville CO-1, CO-4, CO-5, sehemu CO-7, sehemu CO-8 Lubumbashi S-1, S-2, S-13, S-17, S-20 Bandundu B-1, B-10 Gemena E-1, E-14, E-18 Isiro HZ-2, HZ-6, HZ-13, HZ-17, HZ-18 Mbanza Ngungu BZ-3, BZ-4, BZ-6, BZ-7
  • Agosti 16-18 Sandoa sehemu S-5, S-21 Kongolo KI-4, sehemu S-18 Kikwit B-2, B-5, B-8, B-16, B-19, B-20, B-22 Buta HZ-8, HZ-11 Lisala E-8, E-11, E-21
  • Agosti 30-Septemba 1 Kamina S-4, S-6, S-7, sehemu S-15 Tshikapa KA-6, KA-22, KA-23 Kindu KI-3, partie HZ-9, sehemu HZ-16 Lodja KA-4, KA-7, KA-11, KA-12, KA-26, KA-27
  • “Imani Katika Neno La Mungu”
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • “Tembea na Mungu” —Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova wa 2004
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
  • “Neno la Unabii la Mungu” Kusanyiko la Wilaya la Mashahidi wa Yehova 1999
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • “Utii wa Kimungu”—Mkusanyiko wa Wilaya wa Mashahidi wa Yehova wa 2005
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 2/96 uku. 3-4

“Wajumbe Wa Amani Ya Kimungu”

—Kusanyiko La Wilaya 1996

1 Katika 1995 kati ya wale watu 265 750 waliohudhuria kusanyiko la wilaya “Wasifuji Wenye Shangwe” katika eneo letu, wengi ni wale walioonyesha shukrani yao kuhusu yale mawazo yenye kurudisha nguvu kiroho. Mioyo yetu ilijaa shangwe kwa ajili ya wanafunzi 4 318 waliobatizwa kama alama ya kujiweka wakf kwa utu wao kwa Mungu. Tulikuwa wenye furaha kupokea vitabu viwili vipya, Elimu na Mashahidi wa Yehova na Ujuzi Uongozao Kwenye Uhai Udumuo Milele. Jambo la kwamba sisi tuliweza kufaidika na programu ile yenye kusisimua mwaka jana lingepaswa kutusukuma kufanya jitihada zetu zote ili kuhudhuria kwenye kusanyiko la wilaya 1996 “Wajumbe wa Amani ya Kimungu.” Bila shaka sisi sote tutapenda kuwaalika wale ambao hufuatana nasi katika kujifunza Biblia. Kwa kila mmoja wa sisi tupendao kuendelea kumtumikia Yehova kwa shangwe katika siku hizi za mwisho, makusanyiko hayo yatakuwa chemchemi ya vitia moyo na kipaa nguvu kiroho.

2 Mtengeneze mambo yenu vizuri mbele ya wakati ili muweze kuhudhuria kwenye siku tatu za karamu ya kiroho yenye vitu vinono, kuanzia wimbo wa kufungua hadi sala ya kumalizia. Mtakapochukua mipango ili kuhudhuria kwenye kusanyiko, onyesheni upendo kwa kufikiria wale walio na lazima ya msaada, hasa wale wanaopendezwa na kweli karibuni, ili wao pia wawepo kwenye sehemu zote za programu. Ingalikuwa jambo mojapo la lazima kuchunguza maelezo yanayopatikana katika nyongeza hii pamoja na wale watu wanaofuatana nanyi kwa kujifunza Biblia na wanaofikiria kuhudhuria kusanyiko. (Gal. 6:6, 10) Siku ya Tano, kusanyiko litaanza kwa muziki pa saa 3 dakika 30 na litakwisha kuelekea saa 10 dakika 30. Siku ya Posho, litaanza pa saa 3 dakika 30 na litamalizika, wimbo na sala vikitiwa ndani, kuelekea saa 10 dakika 30. Programu ya siku ya Yenga asubui itaanza pa saa 3 dakika 30, pia kusanyiko litamalizika saa 10 hivi. Maelezo yafuatayo yatawasaidia katika matayarisho yenu.

3 Mara nyingi kupokelewa au kupangishwa kunafanyika katika nyumba binafsi za ndugu. Tunapaswa kuwa wenye shukrani kwa akina ndugu na dada hao wanaokubali kutupangisha. Zaidi ya hilo, lingekuwa jambo lisilo sawa kwamba wale wanaofaidika na ukaribishaji-wageni huo waweze kuutumia vibaya kwa kudai kwamba wapangishwe muda mrefu mbele au kisha kusanyiko. Kupangishwa kunatolewa tu WAKATI wa kusanyiko. Wale wanaofaidika na aina hiyo ya kupangishwa wanapaswa kuheshimu mali za wakaribishaji wao, kutoharibu kitu chochote, kutoingia mahali ambapo hawaalikwi kuingia, na kuangalia kwamba watoto wao wafanye vivyo hivyo. Ikiwa wakaribishaji wapambana na tatizo lolote katika hayo, wapaswa mara moja kujulisha hilo kwenye utumishi wa upangishaji wa kusanyiko, ambao watakuwa wenye furaha kutoa msaada wao.

4 Wahubiri wengine, pia watoto wao, wanayo mahitaji ya kipekee; basi yafaa sisi kuwaonyesha utunzaji mzuri. Kutaniko kwa ujumla, pia wazee kwa kipekee, wangepaswa kuangalia vizuri kwamba watu hao washugulikiwe, na si kutwika daraka lao juu ya utumishi wa upangishaji wa kusanyiko. Wazee au washiriki wengine wa kutaniko wanaojua hali yao waweza kuonyesha upendo kwa kuwatolea msaada unaohitajiwa. Mara nyingi jambo hilo ladai kwamba wahubiri wahangaikie mahitaji ya watumishi wa wakati wote, watu wazee-wazee au vilema, nk. Kwa mfano, wanaweza kuwasaidia kwa kuwachukua au kuwatunza kwa njia tofauti.—Yak. 2:15-17; 1 Yn. 3:17, 18.

Wale Watakaohudhuria Kwenye Kusanyiko Lingine

5 Mara nyingi, kusanyiko ambalo kwalo mnaalikwa ni lile lililo karibu na makao yenu. Mipango inachukuliwa kuhusiana na hesabu ya nafasi, vichapo, chakula, kupangishwa, nk., kufuatia kanuni ya kwamba wahubiri wengi watahudhuria kusanyiko ambalo kwalo walialikwa. Lakini, ikiwa kuna sababu yoyote ya maana kwamba mnalazimishwa kuhudhuria kusanyiko lingine tofauti, jisikieni huru kufanya hivyo.

Ushirikiano Wenu ni wa Maana Sana

6 Ili utumishi wa kupangisha uendeshwe vizuri na ufanye kazi yenye matokeo hutegemea ushirikiano wa kila mmoja wenu. (Ebr. 13:17) Ndiyo sababu tunawaomba wote kushirikiana na utumishi wa upangishaji unaowekwa na Sosaiti. Kwa kufanya hivyo, tutapunguza kwa kiasi magumu ambayo sisi hukutana nayo.

 7  Huku tunapojitayarisha kuhudhuria makusanyiko ya wilaya 1996, “Wajumbe wa Amani ya Kimungu,” tukifuatana na ndugu na dada zetu, acheni pia tufikirie tegemezo kwa mali na fedha ambalo tunaweza kuleta kwa matayarisho ya karamu hiyo ya kiroho! Kama ilivyokuwa kwa Waisraeli na wale Wakristo wa kwanza, tusiende huko mikono mitupu.—Tor. 16:​16, 17; 2 Kor. 8:12.

[List of locations on page 4]

MAKUSANYIKO YA WILAYA 1996

TAREHEMAHALIMIZUNGUKO INAYOALIKWA

Julai 5-7 Kinshasa (F) KIN-4, KIN-7, KIN-10

Julai 12-14 Kinshasa (LI-1) KIN-1, KIN-3, KIN-8, KIN-12, KIN-13

Kananga KA-1, KA-14, KA-18, KA-19, KA-28, KA-30

Bujumbura/Uvira KI-8, BU-1, BU-2, BU-3

Malemba Nkulu S-8, S-9, S-10, S-14, S-16

Julai 19-21 Kinshasa (LI-2) KIN-2, KIN-5, KIN-6, KIN-9, KIN-11 Bukavu KI-1, KI-11, KI-12 Ilebo KA-10, KA-15, KA-21, KA-29 Mbuji-Mayi KA-2, KA-5, KA-13, KA-16, KA-17, KA-20, KA-25 Butembo KI-5, KI-7, KI-9, KI-10

Julai 26-28 Bunia HZ-4, HZ-12

Matadi BZ-1, BZ-2, BZ-5, BZ-8

Kasongo Lunda B-7, B-13, B-17

Mbandaka E-2, E-7, E-16, E-17, E-23, E-24

Goma KI-2, KI-6

Mwene-Ditu KA-3, KA-8, KA-9, KA-24

Agosti 2-4 Brazzaville CO-1, CO-4, CO-5, sehemu CO-7, sehemu CO-8 Lubumbashi S-1, S-2, S-13, S-17, S-20 Bandundu B-1, B-10 Gemena E-1, E-14, E-18 Isiro HZ-2, HZ-6, HZ-13, HZ-17, HZ-18 Mbanza Ngungu BZ-3, BZ-4, BZ-6, BZ-7

Agosti 9-11 Kenge B-3, B-9, B-21

Pointe-Noire CO-2, CO-6, sehemu CO-8

Kolwezi S-3, sehemu S-5, sehemu S-15

Nioki B-4, B-6, B-14, B-15

Gbadolite E-5, E-9, E-19

Kisangani HZ-1, HZ-5, HZ-7, sehemu HZ-9, HZ-10, HZ-14,

sehemu HZ-16

Agosti 16-18 Sandoa sehemu S-5, S-21 Kongolo KI-4, sehemu S-18 Kikwit B-2, B-5, B-8, B-16, B-19, B-20, B-22 Buta HZ-8, HZ-11 Lisala E-8, E-11, E-21

Agosti 23-25 Ouesso CO-3, sehemu CO-7

Bumba E-4, E-12, E-15, E-20, E-22, HZ-3, HZ-15

Moba S-11, S-12, sehemu S-18, S-19

Boende E-3, E-6, E-10, E-13, E-25, E-26

Agosti 30-Septemba 1 Kamina S-4, S-6, S-7, sehemu S-15 Tshikapa KA-6, KA-22, KA-23 Kindu KI-3, partie HZ-9, sehemu HZ-16 Lodja KA-4, KA-7, KA-11, KA-12, KA-26, KA-27

Septemba 27-29 Mukedi B-11, B-12, B-18, B-23

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine