Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/96 uku. 7
  • Je! Sisi ni Wenye Shughuli Mno?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je! Sisi ni Wenye Shughuli Mno?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jinsi Ya Kununua Wakati Unaofaa
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Je, Inakuzuia Usihubiri?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Tujenge Maisha Yetu Juu Ya Utumishi Wa Yehova
    Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Tutoe Nafasi Ya Kwanza Kwa Mambo Ya Lazima Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1997
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 6/96 uku. 7

Je! Sisi ni Wenye Shughuli Mno?

1 Paulo alituhimiza kwamba ‘tuzidi kutenda kazi ya Bwana sikuzote.’ (1 Kor. 15:58) Tunatiwa moyo sana kulinda programu ya kila siku ya funzo la kibinafsi, kushiriki kikawaida katika huduma, kuhudhuria kiaminifu kwenye mikutano na kutimiza kwa bidii kazi tunazokabidhiwa katika kutaniko. Bila kusema juu ya msaada tunaopaswa kutoa kwa wale wanaouhitaji. Kwa kuwa na programu kama hiyo, tungeweza wakati mwingine kujisikia kuwa wenye kulemewa na kujifikiria kwamba tunapaswa kutafuta njia za kupunguza kazi zetu.

2 Katika hali fulani, linaweza kuwa jambo la hekima na lenye kufikiri kuzuri kuondoa utendaji kadha au kupunguza kiwango chao. Wengine wanafikiri wanapaswa kufanya kila kitu wanachowaomba. Ukosefu wa usawaziko katika jambo hilo waweza kuwa wenye hatari na chanzo cha msongo na mikazo iwezayo kuangamiza hatimaye.

3 Tuwe Wenye Usawaziko: Kutumikisha shauri la Paulo kwa ‘kuhakikisha mambo yaliyo ya maana zaidi,’ huo ndio ufunguo wa usawaziko. (Flp. 1:10) Hilo humaanisha tu kwamba tukazie akili kikiki juu ya mambo ya muhimu zaidi, kisha, kulingana na wakati unaotubakilia na hali, tushughulike na mambo yaliyo na maana ndogo. Madaraka yetu ya kifamilia yanapatikana bila shaka nafasi nzuri kati ya mambo hayo ya muhimu. Tunapaswa pia kutimiza madaraka fulani ya kimwili. Hata hivyo, Yesu alifundisha kwamba mambo yetu ya kwanza maishani yanapaswa kutegemea kanuni hii: kutafuta kwanza Ufalme. Tunapaswa kwanza kufanya yale yanayohitajiwa ili kutimiza wakfu wetu kwa Yehova.​—Mt. 5:3 ; 6:33.

4 Tukiwa na wazo hilo akilini, tutakuwa waangalifu ili kurahisisha matumizi yetu ya wakati, ambayo tayari ni yenye kujaa, na utendaji wa kibinafsi, viburudisho na ahadi zisizo za lazima kwa wengine. Tunapopanga programu yetu ya juma, tujiwekee kando wakati wa lazima kwa ajili ya funzo la kibinafsi la kutosha, kushiriki kwa kiasi katika huduma, kuhudhuria kwenye mikutano na kwa yote yanayoambatana moja kwa moja na ibada yetu. Wakati unaobaki ungeweza kutumiwa kwa utendaji mwingine kadha, kwa kadiri utendaji huo unavyochangia kufikia mradi wetu wa kwanza, ule wa kuishi maisha ya Kikristo yenye kusawazika yanayoshughulikia kwanza Ufalme.

5 Hata tukifanya hivyo, tungeweza kuendelea kuona mzigo wetu kuwa wenye kulemea. Ikiwa ndivyo, imetupasa kujibu mwaliko wa Yesu: “Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha.” (Mt. 11:​28, NW) Tumwangalie pia Yehova, “[ambaye] siku kwa siku huchukulia mzigo wetu” naye humpa aliyechoka nguvu. Yeye aahidi kwamba hataruhusu mwadilifu apepesuke. (Zab. 55:22 ; 68:19 ; Is. 40:29) Tunaweza kuwa hakika kwamba sala zetu zitajibiwa, zikituwezesha kuvumilia katika maisha yenye matokeo ya utendaji wa kitheokrasi.

6 Ikiwa ni hakika kwamba ufuatiaji wa faida zifaazo za Ufalme unatushughulisha kwa kuendelea, tunaweza kuwa wenye furaha, kwani tunajua kwamba kazi yetu si bure katika Bwana.​—1 Kor. 15:58.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine