Tutoe Nafasi Ya Kwanza Kwa Mambo Ya Lazima Zaidi
1 Ni nini baadhi ya mambo ya lazima yaliyo ya muhimu kwa hali nzuri ya kiroho? Kati ya mambo hayo kuna hasa funzo la kibinafsi, hudhurio kwenye mikutano, kudumu katika sala, mashirika mazuri na huduma ya Kikristo. Hatuwezi kubaki wenye afya nzuri ya kiroho pasipo kuweka mambo hayo ya lazima pa nafasi ya kwanza katika maisha yetu.
2 Hata hivyo, sote tunafanya vita dhidi ya tamaa za mwili na tunahitaji nidhamu. (Gal. 5:17) Hatungepaswa kamwe kufikiri kwamba tungepata faida kwa kufuatia faida zetu za kichoyo. (Yer. 17:9) Hivyo, ikiwa tunataka kulinda moyo wetu na kutokujiacha kupotezwa, ni jambo la lazima tujichunguze kwa ukawaida.—Mit. 4:23; 2 Kor. 13:5.
3 Tuchunguze Moyo Wetu: Kwa hiyo, tunaweza kujiuliza kwelikweli maulizo yafuatayo: Je! ninayo tamaa kubwa ya kusoma Neno la Mungu? (1 Pt. 2:2) Je! ninatambua ulazima wa kuhudhuria kwenye mikutano yote ya kutaniko? (Ebr. 10:24, 25) Je! ninadumu katika sala? (Rum. 12:12) Je! ninatafuta ushirika wa watu wa kiroho? (Rum. 1:11, 12) Je! ninajifanyia kuwa sharti kuhubiri habari njema? (1 Kor. 9:16) Ikiwa tunajibu kwa kuitikia vema, hilo linamaanisha kwamba tunatamani kutoa nafasi ya kwanza kwa mambo yaliyo ya lazima zaidi.
4 Tuchunguze Programu Yetu ya Kila Siku: Ili kutenda kupatana na uchunguzi wa tamaa za moyo wetu, ni jambo la muhimu kwetu kupanga mambo ya kutolea nafasi ya kwanza katika matumizi yetu ya wakati. Hilo linamaanisha, kati ya mambo mengine, kupanga wakati ili kusoma kikawaida Biblia na kila namba ya Mnara wa Mlinzi na Amkeni! na pia kwa ajili ya kutayarisha mikutano. Inafaa pia kuweka wakati kwa ajili ya familia, iwe kwa ajili ya funzo au kwa ajili ya sala ya pamoja. Tuweke mipaka kwa wakati unaotolewa kwenye televisheni au kwenye kompyuta. Tuwe wenye kuazimia kuhudhuria kwenye mikutano yote ya kutaniko na kuiweka mbele ya jambo lingine lolote. Tupange mambo kila juma ili kuhubiri tukiwa familia.
5 Hakuna shaka kwamba tukitoa nafasi ya kwanza kwenye mambo yaliyo ya lazima zaidi katika maisha yetu, tutavuna shangwe.