Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 9/97 uku. 3-4
  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Shirikisho ya Amerika

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Shirikisho ya Amerika
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1997
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Programu ya Ujenzi wa
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Fasi Yetu ya Ibada
    Tengenezo Yenye Kufanya Mapenzi ya Yehova
  • Ibada ya kweli ni yenye kupanuka katika ulaya ya mashariki
    Huduma Yetu ya Ufalme—1999
  • Juu ya Nini Tunajenga Majumba ya Ufalme na Ni Nini Inatusaidia Kuijenga?
    Ni Nani Wanafanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1997
km 9/97 uku. 3-4

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Katika Shirikisho ya Amerika

1 Tunapotupia jicho kwenye kazi ulimwenguni, tunatiwa moyo kwa kuona ongezeko kubwa ambalo tengenezo la kidunia la Yehova linapata. Mwaka wa nyuma, makutaniko 246 yaliundwa katika Shirikisho ya Amerika na, ulimwenguni pote, ni makutaniko 3,288 kwa ujumla yaliyozaliwa. Pamoja na ongezeko la namna hiyo, si jambo la kushangaza kwamba kuwe na uhitaji zaidi wa majumba ya Ufalme zaidi.

2 Ndugu na dada wengi wanaonyesha juhudi ya ajabu na wanategemeza tengenezo la Yehova kwa kutoa kwa kujipendea wakati wao na mali zao katika mpango wa ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Kila moja ya halmashauri za ujenzi za majimbo 75 zilizopo katika Shirikisho ya Amerika inahusika na makutaniko 140 katika eneo inalogawiwa. Kila mwaka, yapata Majumba ya Ufalme 200 yanajengwa na mengine 200 yanarekebishwa upya. Daraka la miradi yote hiyo linaangukia halmashauri za majimbo, na kazi ambayo zinafanya inathaminiwa sana. Yote yanayohusiana na ujenzi wa Majumba ya Ufalme yanaonyesha roho ya Ukristo inayohusu kutoa na kujidhabihu, roho inayotofautiana sana na ile inayotawala katika ulimwengu.—2 Tim. 3:2, 4.

3 Katika kuhangaikia upatano, Sosaiti ilitoa kwa halmashauri za majimbo jumla ya ramani zenye kuchorwa zinazofanana za vielelezo vya Majumba ya Ufalme katika Shirikisho ya Amerika iliyo na ramani kwenye D.A.O. (Dessin assisté par ordinateur.) (Picha inayochapwa na kompyuta).vu avec Didier Rémy Mpango huo unawezesha kukomboa wakati na kutotafuta zaidi wafanyakazi wakujipendea. Unarahisisha pia matumizi yenye akili ya fedha za Sosaiti kwa ajili ya Majumba ya Ufalme. Kwa wakati huu, ni kutokana na ramani hizo za msingi kwamba wazee wanafanya uchaguzi wao. Baada ya kupokea chombo hicho kipya, halmashauri ya jimbo ilisema: “Tulifurahi sana na, kwa kusema yote, kuwa wenye shauku kupokea ramani hizo.  . . . Ndugu wenye maarifa katika mambo yanayohusu ufundi wa ujenzi wa nyumba na ufundi wa ujenzi kwa ujumla wanaona kwamba matumizi ya ramani hizo yanatufanya tukomboe wakati toka asilimia 50 mpaka 60. Hilo linawezesha pia kutunga kanuni zenye kupatana zaidi na zenye kushikamana zaidi kwa ajili ya Majumba ya Ufalme.” Makutaniko yanayoonyesha roho nzuri ya ushirikiano kwa tegemezo layo kwenye ujenzi wa Majumba ya Ufalme yenye kufanana, tunatazamia kwamba gharama ambayo wajenzi wanategemeza kwa kujitoa, mafundi, na pia wafanyakazi kwa mapatano wanaotoa kwa kujipendea msaada wao, uwe mwepesi hata zaidi.

4 Wafanyakazi Wakujipendea Wanategemeza Kazi Bora: Sosaiti ni yenye shukrani kwa wafanyakazi wakujipendea wengi wanaoshiriki katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme. Ni jambo lenye kupendeza kuona makumi ya maelfu ya wafanyakazi wakujipendea kujitoa katika sehemu zote za kazi hiyo. Mafanikio ya programu ya ujenzi yanawezekana kwa sababu ya roho ya kujipendea, ya ukarimu na ya ushirikiano ambayo wafanyakazi wakujipendea wanaonyesha kwa kudhabihu wakati ambao wangeweza kupitisha kwa jambo lingine katika kutaniko lao na pamoja na familia zao. (Zab. 110:​3; Kol. 3:23) Hali hiyo yenye kujaa upendo inastahili pongezi (sifa) zetu, shukrani yetu na tegemezo letu bila kujizuia.—Rom. 12:10; Ebr. 13:1.

5 Inaombwa kwa wale wote wanaojua ufundi mbalimbali kusaidia kikawaida halmashauri za ujenzi za majimbo kujaza fomu ya Ujenzi wa Majumba ya Ufalme​—Karatasi ya maswali kwa wafanyakazi wakujipendea (S-82). Ni kutaniko ndilo linatuma fomu hizo kwenye halmashauri ya jimbo ili kuijulisha kazi wanazojua wafanyakazi wakujipendea na utayari wao. Wakati hali ya mfanyakazi wa kujipendea inabadilika, kwa mfano ikiwa anahama au ikiwa anawekwa rasmi kuwa mtumishi wa huduma au mzee, inafaa kujaza haraka fomu mpya, ambayo itatumwa na mwandishi wa kutaniko. Ikiwa mtu hatimizi matakwa yanayoombwa, wazee wanapaswa haraka kuijulisha halmashauri ya jimbo kwa njia ya barua. Ikiwa mnahitaji fomu zaidi, mtaweza kuziomba kwenye fomu ya kila mwezi Ombi la vichapo (S-14). Mwangalizi wa mzunguko anahusika pia na orodha ya watu wanaojitoa kwa kujipendea katika sehemu hiyo ya utumishi mtakatifu. Anachunguza hivyo upya faili ya karatasi za maswali kwa ajili ya wafanyakazi wakujipendea kila mara anapolitembelea kutaniko.

6 Tupunguze Sana Gharama za Ujenzi: Halmashauri za ujenzi za majimbo zina maagizo ya kupanga utumishi wa ununuzi unaoongozwa na mzee mwenye kujua kazi. Ndugu wanaounda utumishi huo wanachunguza kwa bidii matoleo kwa kusudi la kupata bei nzuri, wanafanya ulinganifu na wanaangalia kwenye kuwa bei ya chini. Katika njia hiyo, tunaweza kujua ni wafanya-biashara gani wataweza kukubaliwa na ni vifaa gani vitaweza kununuliwa. Wakati mwingine, wakati wa kufanya mradi wa Jumba la Ufalme, akina ndugu wa kutaniko wenye kujua kazi wanaalikwa kutoa msaada wao kwa wanamemba wa utumishi huo.

7  Ili kuwa hakika kwamba tunafanya akiba za kutosha iwezekanavyo, gharama zote zinazofanywa juu ya bajeti (makadirio ya matumizi na mapato) ya ujenzi zinapaswa kukubaliwa na halmashauri ya jimbo, ambayo itatia sahihi cheki za benki au risiti. Tangu tu mradi wa ujenzi au wa kurekebisha Jumba la Ufalme fulani unapohitaji msaada wa wafanyakazi wakujipendea wa makutaniko tofauti na yale yatakayokusanyika katika jumba, halmashauri ya jimbo ndiyo inakabidhiwa usimamizi wa mradi.

8 Itaombwa kwa fundi yeyote wa ujenzi anayekubali kwa mapatano kutimiza kazi ya Jumba la Ufalme kutoa ushuhuda kwamba ana bima (fedha inayolipwa baada ya ajali kutukia) kwa ajili ya wafanyakazi wake, na pia bima katika madaraka, na posho ndogo, mapatano hayo yakionyesha kwamba kutaniko linatiwa ndani ya bima na yakiwa na fungu la kukataa.

9 Msaada Wakutolea kwa Matawi Mengine: Inafikia kwamba matawi mengine yana uhitaji wa msaada wa halmashauri za ujenzi za majimbo za Shirikisho ya Amerika. Ndivyo ilivyo mara nyingi wakati inapohusu kutengeneza hasara zilizosababishwa na maafa fulani au ili kutoa mazoezi kwa wanamemba wa halmashauri ya ujenzi ya jimbo ya mahali. Ndugu walio na madaraka kwa upande huo na walio tayari kwenda ugenini, kwa fedha yao, ili kusaidia halmashauri nyingine wanatoa ushuhuda nzuri wa upendo. Wakati ombi linalofanywa kupitia tawi linapokubaliwa, Sosaiti inaita halmashauri ya jimbo ambayo labda programu ya ujenzi katika eneo layo ni nyepesi katika kipindi hicho. Hivyo, mambo yanapangwa vizuri.

10 Kwa kuwa uhitaji wa Majumba ya Ufalme katika nchi nyingine unazidi kuongezeka, ni jambo la lazima kutumia kihekima iwezekanavyo fedha zilizopo. Barua ya Juni 15, 1995 iliyotumwa kwa makutaniko yote ya Shirikisho ya Amerika ilitutia moyo kufanya akiba kwa kadiri kubwa katika ujenzi au urekebishaji wa majumba. pas trouvée ? ? ? Ombi hilo lilipata kuitikiwa vizuri sana. Kinyume na hilo, kama ilivyotangazwa na Huduma Yetu ya Ufalme ya Machi 1997 (Shirikisho ya Amerika), aucune mention dans le km filiales ni le km France !sehemu moja ya fedha za Sosaiti kwa ajili ya Majumba ya Ufalme inawekwa akiba sasa kwa mikopo inayotolewa kwa makutaniko ya nchi fulani ambako uhitaji katika majumba ni mkubwa sana, lakini ambayo mapato si mengi na ambayo yako katika hali ngumu ya kiuchumi.

11 Kitabu-Mwaka 1997 kinatia mkazo juu ya ulazima wa kuwa na majumba zaidi katika nchi fulani. Kuna nchi, kama vile, Ukrania ambako Majumba ya Ufalme 47 yalijengwa mpaka sasa, na ambako mengine 56 yanaendelea bado kujengwa. Ni wazi kwamba kuna uhitaji katika nchi hizo. Ni yale yanaonyeshwa na ripoti moja: “Katika Urusi, kunahitajiwa majumba zaidi. Kuongezeka kwa hesabu ya Mashahidi ni kwa haraka sana, lakini yapata asilimia 85 ya makutaniko yanayoangaliwa na tawi la Urusi hayana mahali pa mikutano pa kawaida. Katika Zimbabwe, ambako kuna makutaniko 800, mengi yayo yanalazimika kukusanyika nje. Matokeo ni kwamba, watu fulani walioonyesha kupendezwa hivi karibuni wanajizuiza kuhudhuria kwenye mikutano.” Hali kama hizo zinapatikana katika Ulaya ya Mashariki, katika Afrika na katika Amerika ya Kilatini.

12 Hakika, katika siku hizi za mwisho, upendo wa wanadamu wengi unapoa, lakini wale wanaofanyiza taifa la Mungu wanaendelea kuonyesha upendo wao wamoja kwa wengine, upendo unaotupilia mbali mipaka ya rangi ya ngozi au ya maeneo. (Mt. 24:12) Tukiwa wenye kumwiga Baba yetu wa mbinguni, basi na tuendelee kuonyesha upendo wa namna hiyo kwa kutegemeza kwa kujipendea wenyewe ujenzi wa Majumba ya Ufalme, iwe katika Shirikisho ya Amerika kama vile ugenini! Kwa kutenda hivyo, tutajiletea ukubali na baraka nyingi za Yehova.—Mal. 3:10; Ebr. 6:10.

[Box on page 4]

Ujenzi wa Majumba ya Ufalme Ulimwenguni

1 Uhitaji wa Majumba ya Ufalme ni mkubwa ulimwenguni pote. Mnamo mwaka wa utumishi 1996, kuliundwa si chini ya makutaniko 3,288 ambayo hesabu kubwa ni katika Afrika, katika Amerika ya Kati, katika Amerika ya Kusini, katika Asia na katika Ulaya ya Mashariki.

2 Chapa zilizotangulia za Huduma Yetu ya Ufalme zilitoa ripoti juu ya maendeleo yaliyofanywa katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme katika nchi nyingi. Hata hivyo, ripoti zinaonyesha kwamba kuna tu Jumba la Ufalme moja katika nchi inayohesabu makutaniko 568. Katika nchi nyingine, kunahesabiwa Jumba la Ufalme 1 kwa makutaniko 129. Mahali pengine tena, ulinganifu ni wa jumba 1 kwa makutaniko 41. Katika nchi nyingine nyingi zinazohesabu kwa ujumla zaidi ya makutaniko 1,000, haikuwezekana kujenga hata Jumba la Ufalme moja, na hilo kwa sababu ya magumu ya kiuchumi. Kazi kubwa imekwisha kutimizwa, lakini kuna bado mengi ya kufanya. Tupo hakika kwamba ndugu wa Shirikisho ya Amerika wangependa kuyasaidia makutaniko ya ugenini yasiyokuwa na Majumba ya Ufalme yenye kustahili.

3 Hii inalingana na 2 Wakorintho 8:​14, linalosema: “Kupitia usawaziko wa ziada yenu sasa hivi ipate kujazia upungufu wao.” Katika nchi nyingi kumeundwa mfuko wa fedha kwa ajili ya Majumba ya Ufalme, lakini hali ya kiuchumi hairuhusu akina ndugu kujenga majumba mengi ambayo mahitaji yangeomba. Hata hivyo, kwa msaada wa ndugu wa nchi nyingine, Sosaiti iliweza kutegemeza ujenzi wa Majumba ya Ufalme 413 na kurekebisha mengine 727 katika yapata nchi tofauti 75, na hilo katika majuma manne tu. Kwa kuwa maombi yanabaki tu kuwa ni mengi, ni jambo la lazima kuchukua katika akiba yetu fedha kwa ajili ya Majumba ya Ufalme ili kutegemeza ujenzi ugenini. Tunapoendelea kutoa mikopo kwa ajili ya ujenzi wa majumba ambayo yanahitajiwa katika Shirikisho ya Amerika, kwa kadiri mahitaji yanavyotimizwa na fedha hupatikana, tutatumia pia fedha zetu ili kuyasaidia makutaniko mengine ya nje. Tunafurahi kuhudhuria kwenye ujenzi wa Majumba ya Ufalme zaidi ulimwenguni pote, kwa sifa ya Yehova.—Zab. 102:16; Hag. 1:7, 8.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine