Tuhubiri Kwa “Watu Wa Namna Zote”
1 Tunapokutana na watu wa tamaduni tofauti tofauti na elimu za kidini tofauti tofauti, tunakumbuka vema ya kuwa Yehova anataka “kwamba watu wa namna zote waokolewe na kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.” (1 Tim. 2:4) Zaidi ya trakti mbalimbali na broshua zilizoandikwa kipekee kwa kusudi hilo, tunavyo vitabu viwili bora tunavyoweza kutumia wakati wowote ule ili kusaidia watu ambao dini yao haikuwafundisha kweli juu ya Mungu na Yesu.
2 Kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kinatoa mwono wa namna dini kubwa za ulimwengu zilivyoanza; hivyo, kinaweza kuwasaidia watu kutoka mahali mbalimbali wafanye ulinganifu kati ya imani zao na kile ambacho Biblia hufundisha juu ya Mungu pekee wa kweli. Au, kwa kuvuta uangalifu juu ya maisha ya Yesu Kristo, kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi Aliyepata Kuishi kinaweza kusaidia mtu kumjua vizuri zaidi Mwana wa Mungu na kuvutwa naye, kama walivyofanya watu wengi katika karne ya kwanza. (Yn. 12:32) Kila wakati tutakapoona hilo kuwa lenye kufaa, tujaribu basi madokezo yafuatayo ili kutolea vitabu hivyo:
3 Ikiwa tunafikiri kwamba ingekuwa vizuri kutolea kitabu “Yule Mtu Mkuu Zaidi,” tuulize swali hili:
◼ “Ni wazo gani linalokuja akilini mwako unapofikiri juu ya Yesu Kristo? [Tuache mtu ajibu.] Wanahistoria wengi wanakubali kwamba Yesu alikuwa ndiye mtu mkuu zaidi aliyepata kuishi. [Tutaje mfano tutakaoupata kwenye utangulizi wa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi.] Biblia inaonyesha kwamba maisha ya Yesu ni kielelezo cha kuigwa na wanadamu.” Tusome 1 Petro 2:21 na fungu la kwanza la ukurasa wa mwisho wa utangulizi wa kitabu Yule Mtu Mkuu Zaidi. Ikiwa msikilizaji wetu anatamani kujifunza mengi juu ya Yesu, tumtolee kitabu. Kabla ya kuondoka, tusome Yoane 17:3 na tuulize: “Tunawezaje kutwaa ujuzi huu uongozao kwenye uhai udumuo milele?” Tuchukue mipango kamili ili kurudi kumtolea jibu kwa ulizo hilo.
4 Wakati wa ziara ya kurudia, ili kufasiria jinsi ya kutwaa ujuzi sahihi unaotoa uhai, tunaweza kusema kwa mfano:
◼ “Niliahidi kurudi ili kukuonyesha namna tunaweza kutwaa ujuzi uongozao kwenye uhai udumuo milele.” Tutoe kitabu Ujuzi, na tuonyeshe msikilizaji wetu namna funzo linavyoendeshwa kwa kutumia sura ya kwanza.
5 Ikiwa tunatamani kutoa kitabu “Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu,” tuanze kwa kuuliza swali lifuatalo:
◼ “Leo kuna dini nyingi sana: je! umekwisha kujiuliza jinsi ya kutambua ile ambayo Mungu anakubali?” Baada ya kusikiliza jibu, tufungue kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu kwenye ukurasa 377. Tutokeze nukta ya 7, na tumuulize msikilizaji wetu ikiwa yeye pia anafikiri kwamba dini ya kweli ingepaswa kuunganisha wanadamu wote wenye rangi za ngozi tofauti. Tuchukue moja ya maandiko yanayotajwa, na ikiwa wakati unaruhusu, tutoe maelezo juu ya nukta nyingine ya orodha hiyo. Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa kwa kweli, tumtolee kitabu. Wakati wa kuondoka, tunaweza kuamsha ulizo lifuatalo: “Dini ya kweli ingepaswa kuwa na uvutano gani juu ya mwenendo wa washiriki wayo?” Tuchukue mipango ili kujibu ulizo hilo.
6 Tunaporudi kufasiria uvutano ambao dini ya kweli inapaswa kuwa nao juu ya maisha ya washiriki wayo, tunaweza kuuliza:
◼ “Kwa maoni yako, je! dini ilipaswa kuwa na uvutano juu ya mwenendo wa washiriki wayo? [Tuache mtu ajibu.] Kristo alitutolea kanuni ambayo kwa hiyo mtu anaweza kuamua juu ya dini.” Tusome Mathayo 7:17-20 moja kwa moja kwenye kurasa 12 na 13 za kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu. Kisha tumwombe mtu asome fungu 20 kwenye kurasa 13 na 14. Ikiwa tunao wakati, tuzungumzie mafungu 25-9 kwenye kurasa 16-18. Hivyo, tunaweza labda kuanzisha funzo kwa kutumia, ama broshua Anataka, ama kitabu Ujuzi.
7 Namna ya Kuanzisha Mazungumzo: Kuna vifaa vingi vya ufundishaji katika kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu, ambavyo vinaweza kutusaidia kuanzisha mazungumzo, ama wakati wa ziara ya kwanza, ama ule wa ziara inayofuata. Tunaweza kuanza mazungumzo kwa kuuliza tu ulizo lenye akili. Kwa mfano, hapa ni maulizo na vichwa vya habari vilivyochaguliwa ambavyo habari yavyo zaidi inapatikana kwenye kurasa zinazoonyeshwa hapa:
“Maswali Yanayotaka Jibu”: kurasa 17-18
“Je! Yesu Alikuwa Ngano Tu?”: ukurasa 237
“Nani Aliandika Biblia?”: ukurasa 241
“Qurani na Biblia”: ukurasa 285
“Uthibitisho wa Uasilia wa Biblia”: kurasa 340-1
“Wanayoamini Mashahidi wa Yehova”: kurasa 356-7
“Jinsi ya Kutambua Dini ya Kweli”: ukurasa 377
8 Tunaweza kwenda kwenye kurasa zilizochaguliwa za kitabu Jitihada ya Ainabinadamu ya Kutafuta Mungu na kufasiria wazo linalochunguzwa. Kisha tupange siku tutakaporudi kwa kuuliza ulizo linaloambatana na habari iliyozungumziwa na ambalo tutaweza kujibu labda kwa broshua Anataka, labda kwa kitabu Ujuzi. Tusisahau kumwalika mtu kwenye mkusanyiko wa watu wote na kumwachia mwaliko.
9 Watu wanyofu wa namna zote hutafuta kweli juu ya Mungu na Kristo. Tunaweza kuwasaidia wakati wa utendaji wetu wa kutoa ushahidi. Kwa hiyo, tuendelee ‘kufanya kazi kwa bidii na kujikakamua wenyewe, kwa sababu tumeweka tumaini letu juu ya Mungu aliye hai, ambaye ni Mwokozi wa namna zote za watu.’—1 Tim. 4:10.