Aprili—wakati wa kuwa wenye bidii kwa kazi zilizo bora!
1 Wakati tufani (upepo mkali) inapokaribia eneo lenye kukaliwa, uhitaji wa kuonya watu kuhusu hatari hiyo huwa wa haraka. Kadiri tufani inavyokaribia zaidi na zaidi, maonyo yanapaswa kutolewa kwa mkazo zaidi. Kwa nini? Kwa kuwa uhai unahusika! Huenda watu fulani hawakusikia maonyo ya kwanza. Huenda wengine waliyasikia lakini wakapuuza kutenda. Hilo ni kweli kuhusiana na onyo la kimungu ambalo tumeamuriwa kutoa kabla ya “upepo wa kuzunguka” wa hasira yenye uadilifu ya Mungu kuondolea mbali sehemu zote za ulimwengu huu mwovu. (Mez. 10:25) Uhai wa milele wa mamilioni ya watu unahusika! Onyo linapaswa kutolewa. Tunapaswa kuwa “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.”—Tito 2:11-14.
2 Kwa makumi mengi ya miaka, watu wa Yehova wamechochewa kufanya kipindi cha Ukumbusho kuwa wakati wa bidii ya pekee katika huduma. Katika masika ya 1939, Informant, iliyotangulia Huduma Yetu ya Ufalme, ilitoa kitia-moyo kifuatacho: “Masika yakiwa yenye kukaribia, na hali ya hewa yenye kufaa, tunapaswa kutazamia wahubiri [wa kutaniko] wazidishe mara mbili saa shambani, na mapainia waongeze wakati wao vya kutosha. Aprili ni mwezi wenye Siku ya Yenga tano. Huo una Siku ya Posho tano pia. Fanyeni kila Siku ya Posho na Siku ya Yenga mnamo Aprili . . . kuwa wakati kwa ajili ya kutoa ushahidi kwa namna ya pekee.” Huo ulikuwa mradi wenye mwito wa kushindana uliotolewa kwa akina ndugu miaka 60 iliyopita! Mwaka huu, kama vile tu mnamo 1939, mwezi wa Aprili una miisho-juma kamili mitano. Mipango yako ni gani mwezi huu? Ni maandishi gani ambayo umefanya juu ya kalenda yako kwa ajili ya Aprili 2000? Chukua mipango ili kushiriki vya kutosha katika kazi zilizo bora pamoja na watu wengine wa Yehova mnamo mwezi huu wa pekee wa utendaji wa kiroho wenye kuharakishwa.
3 Yale tunayotumaini kutimiza: Siku ya maana zaidi ya mwaka 2000 inaanguka katika mwezi huu. Hiyo ni Aprili 19, ukumbusho wa kila mwaka wa kifo cha Yesu. Acheni tufanye jitihada ya pekee ili kualika watu wengi zaidi iwezekanavyo kwenye Ukumbusho. Kama ilivyodokezwa mwezi uliopita, fanya orodha ya wale wote wanaoweza kuhudhuria Ukumbusho na uhakikishe kwamba hata mmoja hakusahauliwa. Wale walioalikwa wapasa kutia ndani wahubiri wowote wasiotenda, wanafunzi wa Biblia, ziara za kurudia, wale ambao walijifunza hapo mbele, wafanyakazi wenzako, washiriki wenzako wa shule, majirani, watu wa jamaa, na watu wengine unaojuana nao. Je, wale wanaotaka kuhudhuria wana namna ya kusafiri? Ikiwa sivyo, je, unaweza kusaidia kwa upendo? Usiku wa Ukumbusho, sisi sote tutakuwa na pendeleo la kufanya wale wenye kuhudhuria wajisikie kuwa wenye kukaribishwa. Baada ya Ukumbusho, tunaweza kuendelea kutolea hao wenye kupendezwa msaada wa kiroho wa ziada.
4 Kuwa “wenye bidii kwa kazi zilizo bora” siku za kabla na baada ya Ukumbusho ni njia nzuri ya kuonyesha Yehova kwamba tunathamini kwelikweli yale yote ambayo amefanya kwa ajili yetu. Wengi wetu watakuwa na uwezo wa kuongeza jitihada zetu katika utendaji wa kueneza evanjeli. Ikiwa wewe ni painia msaidizi, utataka kufanya yote uwezayo ili kupitisha saa 50 au zaidi katika huduma. (Mt. 5:37) Shikamana na programu uliyopanga mwanzoni mwa mwezi. (Mhu. 3:1; 1 Kor. 14:40) Acheni wengine wetu tufanye yale tuwezayo ili kutoa mkono wenye utegemezo kwa mapainia wote, kwa kuwatia moyo na kwa kutumika nao shambani. (Linganisha 2 Wafalme 10:15, 16.) Ikiwa tunapanda kwa bidii mnamo Aprili, tunaweza kutazamia furaha kubwa na baraka kutoka kwa Yehova. (Mal. 3:10) Huenda hilo litafungua njia kwa upainia msaidizi au upainia wa kawaida wenye kuendelea. Mwendo huo wa kiroho tunaoanzisha mnamo Aprili na uendelee katika miezi itakayofuata kadiri tunavyoendelea kuwa wahubiri walio kawaida wa Ufalme.
5 Hakuna shaka kwamba mwezi huu maelfu ya watu wa Yehova wataanzisha mafunzo mengi ya Biblia ya nyumbani. Je, ungependa kuanzisha moja? Sali kipekee kwa ajili ya funzo, na utende kwa kupatana na sala zako. Unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atathamini maombi yako yenye unyenyekevu ya kupata mtu mwenye moyo mnyofu utakayemfundisha.—1 Yn. 3:22.
6 Ufuatao ni utoaji ambao umejaribiwa shambani na ambao umetumiwa kwa matokeo ili kuanzisha mazungumzo. Unaanza kwa kuuliza: “Je, unafikiri kwamba jeuri yote na ukosefu wa adili kingono katika shule za watu wote ni tokeo la utendaji wa kishetani, au je, huo unatokana na ukosefu wa mazoezi ya wazazi?” Acha mtu ajibu. Ikiwa mtu anasema “utendaji wa kishetani,” soma Ufunuo 12:9, 12, na uonyeshe daraka la Ibilisi katika kuendeleza msukosuko ulimwenguni. Kisha, fungua broshua Anataka kwenye somo 4, na uulize ikiwa mtu amekwisha kujiuliza Shetani alitoka wapi. Anza kusoma na kuzungumzia mafungu mawili ya kwanza. Ikiwa mtu anachagua “ukosefu wa mazoezi ya wazazi” kuwa sababu ya jeuri na ukosefu wa adili kingono katika shule, soma 2 Timotheo 3:1-3 na uonyeshe tabia ambazo bila shaka huchangia katika tatizo hilo. Kisha, fungua broshua Anataka kwenye somo 8, soma fungu 5, na uendelee na mazungumzo. Ikiwa unaweza kupatana na mtu ili kurudi, unaweza hivyo kutayarisha njia kwa ajili ya funzo la Biblia la kawaida pamoja naye. Wakati wa ziara ifuatayo, mwulize ikiwa anajua mtu mwingine yeyote anayeweza kupendezwa kusikia yale anayojifunza.
7 Njia nyingine ya kuwa “wenye bidii kwa kazi zilizo bora” mnamo Aprili ni kushiriki katika aina zote za mahubiri. Je, umekuwa ukifikiria kutoa ushahidi katika shamba la wanyama au mahali pa kuegeshea magari? Kwenye kituo cha basi au kwenye stesheni ya gari-moshi? Sokoni au kwenye shirika la simu? Au je, ungetaka kujaribu kutoa ushahidi kwa njia ya simu, barabarani, au katika eneo la biashara? Kwa nini usitumikishe mawazo hayo mwezi huu? Yehova atakusaidia kuwa na ujasiri unaohitajiwa. (Mdo. 4:31; 1 Thes. 2:2b) Labda unaweza kupatana kutumika na painia au mhubiri mwenye ujuzi katika pande hizo za huduma.
8 Yeyote anayetaka kuongeza ushirika wake katika kazi ya kutoa ushahidi atataka kushiriki katika kutoa ushahidi wa vivi hivi. Mara nyingi, yote inayohitajiwa ni kuhusisha mtu katika mazungumzo ya kirafiki. Tokeza tu habari yenye kupendeza watu wote, labda kwa kutumia utoaji unaoonyeshwa katika fungu 6. Jitahidi kufanya matumizi mazuri ya hata sehemu ndogo-ndogo za wakati ambao, kwa njia nyingine, ungepotea. Hatutupilii mbali senti 5, 10 au 20 ati kwa sababu tu hizo si noti za franka yenye kuenea. Kwa nini usitumie ifaavyo hata dakika tano, dakika kumi, au robo ya saa ukitoa ushahidi wa vivi hivi?
9 Wakati wa kutafakari: Rudi nyuma ili kufikiria nukta zilizotolewa kwa nguvu katika drama kwenye Mkusanyiko wa Wilaya “Neno la Mungu la Kiunabii,” mwaka uliopita. Drama, iliyokuwa na kichwa Kuthamini Urithi Wetu wa Kiroho, ilitufanya tufikiri kwa uangalifu juu ya tofauti kati ya Yakobo na Esau. Esau alisema kwamba, kama Yakobo, yeye alipendezwa na mambo ya kiroho, lakini matendo ya Esau hayakuonyesha hivyo. (Mwa. 25:29-34) Ni onyo lenye nguvu kwetu kama nini! Kama Yakobo, acheni tuwe tayari kujitahidi, hata kupigana, kwa ajili ya baraka ya Yehova. (Mwa. 32:24-29) Kwa nini tusitumie Aprili na miezi mingine yote yenye kufuata ili kufanya upya bidii yetu, huku tukiwa wasiokosa kamwe uthamini kwa urithi wetu mzuri ajabu wa kiroho?
10 “Siku kubwa ya BWANA [Yehova, NW] ni karibu, ni karibu na inafanya mbio sana.” (Zef. 1:14) Habari njema ya Ufalme inapaswa kutolewa. Uhai unahusika! Mwezi huu na uonekane kuwa wenye kubarikiwa kipekee kwa ajili ya watu wa Yehova wote kadiri tunavyoonyesha kwa umoja kwamba sisi ni “wenye bidii kwa kazi zilizo bora.”
[Box on page 4]
Mwaka huu, mwadhimisho wa Ukumbusho utafanyika Siku ya Tatu, Aprili 19. Wazee wanapaswa kutoa uangalifu kwa mambo yafuatayo:
Mambo ya kutosahau kwa ajili ya ukumbusho.
◼ Katika kupanga wakati kwa ajili ya mkutano huo, hakikisheni kwamba mifano haitapitishwa kabla ya jua kutua.
◼ Kila moja, kutia ndani msemaji, anapaswa kujulishwa wakati kamili na mahali pa mwadhimisho huo.
◼ Aina yenye kufaa ya mkate na divai lazima vipatikane na kufanywa viwe tayari.—Ona Mnara wa Mlinzi wa Machi 1, 1985, ukurasa 17.
◼ Sahani, bilauri, na meza yenye kufaa na nguo ya mezani lazima viletwe kwenye jumba na kupangwa mbele ya wakati.
◼ Jumba la Ufalme au mahali pengine pa mkusanyiko huo lazima pasafishwe kikamili kabla ya wakati.
◼ Wakaribishaji na wahudumu wanapaswa kuchaguliwa na kupewa maagizo mbele ya wakati kuhusu kazi yao na utaratibu wenye kufaa.
◼ Mipango lazima ifanywe ili kuhudumia mpakwa-mafuta yeyote asiyejiweza au asiyeweza kuwako.
◼ Ikiwa makutaniko mengi yamepanga kutumia Jumba la Ufalme lilelile, lazima kuwe usawazishaji wenye kufaa kati ya makutaniko ili kuepuka msongamano usiohitajika katika sebule au mwingilio, kwenye njia za waendao kwa mguu, na mahali pa kuegeshea magari.