Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/01 uku. 1
  • Tukuzeni Yehova kwa matendo mema

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tukuzeni Yehova kwa matendo mema
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2001
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Je, Una “Bidii kwa Ajili ya Kazi Njema”?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Tutiane Moyo kwa Bidii Katika Matendo Mazuri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • ‘Iweni Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora’
    Huduma Yetu ya Ufalme—2002
  • Kutoa Ushahidi Bila Neno
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2001
km 2/01 uku. 1

Tukuzeni Yehova kwa matendo mema

1 Wakati unaponaswa katika upepo mbaya wenye nguvu nyingi, ni jambo lenye kutuliza kama nini kuweza kupata mahali pa salama! Ikiwa ndani kuna joto na usalama, na ikiwa wakaaji wa mahali hapo ni wakaribishaji-wageni, utafurahi kubaki hapo. Kazi ya kuhubiri Ufalme inaongoza watu mahali kama hapo pa salama kutoka mfumo wa Shetani. Je, mwenendo wetu wa kila siku unaweza kusaidia wengine waone jinsi mahali hapo salama panavyotoa kichocheo? Ndiyo, kwa kuwa Yesu alisema kwamba watu ‘wangepata kuona matendo yetu mema, na kumtukuza Baba yetu aliye mbinguni.’—Mt. 5:16, Biblia Takatifu.

2 Tunaweza kujiendeshaje ili matendo yetu yavute wengine kwa Yehova na kwa tengenezo lake? Kwa kuacha maneno ya Yesu yanayoandikwa kwenye Luka 6:31 na 10:27 yatengeneze maisha yetu kila siku. Hilo litatuchochea tuonyeshe kwamba tunahangaikia kwa upendo wanadamu wenzetu, nalo litatutofautisha na ulimwengu huu wenye baridi na usiojali.

3 Dada mmoja katika chombo cha baharini aliona mwanamke kijana ambaye aligonjwa sana kwa sababu ya kusafiri majini hivi kwamba hakuwa na uwezo wa kushughulikia mtoto wake mchanga. Dada huyo akaomba ashughulike na mtoto. Wakati mwanamke huyo alipouliza jinsi angeweza kuonyesha shukrani zake, dada akasema: ‘Tafadhali, sikiliza Mashahidi wa Yehova wakati ujao watakapokutembelea.’ Mwanamke huyo alifanya hivyo, na sasa yeye na mume wake ni Mashahidi. Matendo mema yalifanya waitikie ujumbe wa Ufalme kwa njia tofauti.

4 Maisha yetu yote yanahusika: Mwenendo wetu kati ya majirani, tunapokuwa kazini au shuleni, na muda wa vipindi vya kujiburudisha unafanya wengine wawe na maoni fulani kuhusu sisi na kuhusu dini yetu. Kwa hiyo, tunapaswa kujiuliza: ‘Watazamaji wananionaje mimi na familia yangu? Je, majirani wanaona nyumba yetu na uwanja wetu kuwa safi na wenye kutunzwa vizuri? Je, wafanyakazi na wanashule wenzetu wanatuona kuwa wenye kufika pa wakati na wenye bidii? Je, wengine wataona hali yetu ya nje kuwa yenye kiasi na yenye adabu?’ Matendo yetu mema yanaweza kufanya ibada ya Yehova iwe yenye kuvutia zaidi kwa wengine.

5 Petro alionya kwamba Wakristo wangekuwa wenye kudhihakiwa. (1 Pet. 4:4) Tunapaswa kuwa hakika kwamba mwenendo wetu hautokezi maneno yasiyofaa. (1 Pet. 2:12) Ikiwa matendo yetu ya kila siku yanatukuza yule Mungu tunayemwabudu, tutakuwa kama vile taa zenye kuwekwa juu, zikivuta wengine waje mahali pa salama ambapo Yehova anatoa.—Mt. 5:14-16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine