Iweni wenye “kushughulika kwa juhudi nyingi” na huduma yenu
1 Wakati tunaposoma kwamba mtume Paulo alitumika kwa kutengeneza hema wakati alipokuwa Korintho, tunaweza kudhani kwamba hilo lilipunguza nafasi yake ya kuhubiri. Lakini, andiko la Matendo 18:5 linaeleza: “Paulo alianza kushughulika kwa juhudi nyingi na lile neno, akiwatolea Wayahudi ushahidi ili kuthibitisha kwamba Yesu ndiye Kristo.” Kwa nini Paulo alishughulika sana na utendaji wa kuhubiri? Ingawa wengi katika Korintho walikuwa tayari wamekuwa waamini, Bwana alihakikisha kwamba bado kulikuwa watu wengi ambao walipaswa kufanywa kuwa wanafunzi katika mji huo. (Mdo. 18:8-11) Je, tunayo sababu yenye kufanana na hiyo ya kushughulika kwa juhudi nyingi na huduma yetu? Ndiyo. Watu wengi zaidi wanaweza kupatikana na kufundishwa kweli.
2 Pitisheni wakati mwingi zaidi katika huduma mnamo Aprili: Yaelekea kwamba ni mradi wako kuendelea kuwa mwenye shughuli katika kuhubiri habari njema kila mwezi. Lakini miezi fulani hututolea nafasi nyingi zaidi za “kushughulika kwa juhudi nyingi” na utendaji huo. Hiyo inatia ndani mwezi wa Aprili, kwenye upeo wa kipindi cha Ukumbusho. Je, hali zako zimekuruhusu kuwa painia msaidizi au kuongeza jitihada yako katika huduma mnamo kipindi hicho? Wahubiri wengi wanaofanya hivyo wamebarikiwa sana. (2 Kor. 9:6) Ikiwa unafanya yote uwezayo, kumbuka kwamba Yehova anapendezwa na utumishi wako wa moyo wote. (Luka 21:2-4) Hata hali zako ziwe nini, jiwekee mradi wa “kushughulika kwa juhudi nyingi” na huduma yako mnamo Aprili. Na usisahau kutoa ripoti yako ya utumishi wa shambani mwishoni mwa mwezi kusudi jitihada yako ihesabiwe pamoja na ile ya watu wengine wa Yehova.
3 Tembeleeni wapya waliohudhuria ukumbusho: Katika eneo la tawi letu mwaka uliopita, hudhurio kwenye Ukumbusho lilikuwa 604,160. Jumla ya hudhurio la mwaka huu haijajulikana bado. Hata hivyo, ripoti zinaonyesha kwamba kuna uwezekano wa ajabu wa kupata “mavuno” makubwa zaidi. (Mt. 9:37, 38) Kwa hiyo, mapema zaidi iwezekanavyo, chukueni mipango ili kutembelea wale wenye kupendezwa waliohudhuria Ukumbusho ili kuwasaidia kiroho. Kuweka ziara hizo nyuma pa wakati ujao kunaweza kuruhusu ‘yule mwovu kuja na kunyakua neno la Ufalme lililopandwa mioyoni mwao.’ (Mt. 13:19) Ziara inayofanywa upesi itaonyesha kwamba kwa kweli nyinyi ni wenye “kushughulika kwa juhudi nyingi” na huduma yenu.
4 Endeleeni kusaidia wale wasiotenda: Mnamo Februari, jitihada ya pekee ilianza ili kusaidia wale wasiotenda. Ikiwa kuna wengine ambao bado hawajapokea ziara ya uchungaji, wazee wanapaswa kuchukua mipango ili kuwatembelea mbele kabisa ya Aprili kwisha. Wazee watajitahidi kuamua sababu kubwa ya tatizo la mtu na jinsi ya kumsaidia kwa njia bora zaidi ili atumikie Yehova kwa kutenda tena. Msaada huo wenye upendo unaonyesha kwamba wazee wanachukua kwa uzito daraka lao wakiwa wachungaji wa “kundi la Mungu.” (1 Pet. 5:2; Mdo. 20:28) Toleo la Mnara wa Mlinzi la Septemba 15, 1993, kurasa za 22-3, linatoa madokezo bora yanayoweza kutumiwa na wazee wakati wanapozungumzia yoyote ya yale matatizo matano ya mfano ambayo huenda yakawa na uvutano juu ya wale wasiotenda. Tunafikiri kwamba wengine bado wanaweza kufanywa wawe wenye kutenda katika huduma ya shambani mnamo Aprili.
5 Saidieni wengi zaidi wawe wahubiri wasiobatizwa: Je, watoto wenu wametimiza matakwa ya kuwa wahubiri wapya wa habari njema? Namna gani kuhusu wengine mnaojifunza Biblia pamoja nao? Ikiwa hao wanakubaliwa na wazee, je, mwezi wa Aprili haungekuwa wakati wenye kufaa kwao kuanza kuhubiri? Ikiwa mtu fulani ni mwenye kufanya maendeleo na kwamba amejifunza broshua Anataka na kitabu Ujuzi, funzo la Biblia linaweza kuendelezwa katika kitabu cha pili—kitabu Neno la Mungu, kitabu Amani ya Kweli, au kitabu Wenye Umoja Katika Ibada. Mradi wenu ni kusaidia mwanafunzi afikie ufahamu wenye kina kirefu zaidi wa kweli, atimize matakwa ya kuwa mhubiri asiyebatizwa, na awe Shahidi wa Yehova, aliyejiweka wakfu na aliyebatizwa.—Efe. 3:17-19; 1 Tim. 1:12; 1 Pet. 3:21.
6 Kupendezwa na wanafunzi wenu wa Biblia kwa njia yenye upatano na ya kweli kunaweza kuwasaidia mwishowe wafanye kweli kuwa mali yao wenyewe. Shahidi mmoja wa kiume alikutana na mume na mke wazee-wazee wenye kuoana ambao kwa moyo wote walikubali funzo la Biblia. Lakini mume na mke hao waliweka funzo nyuma pa wakati ujao muda wa majuma matatu yenye kufuatana. Mwishowe funzo lilianzishwa. Kisha, mume na mke hao walifuta funzo karibu kila juma baada ya hapo. Hata hivyo, mwishowe mke akafanya maendeleo kufikia ubatizo. “Baada ya yeye kubatizwa,” ndugu akumbuka, “macho yake yalijaa machozi ya furaha, jambo lililotokeza machozi ya furaha kwangu na kwa mke wangu.” Ndiyo, “kushughulika kwa juhudi nyingi” na habari njema huleta furaha kubwa!
7 Unabii wa Biblia na matukio ya ulimwengu vinaonyesha kwamba tunaishi wakati wa mwisho kabisa. Sasa ndio wakati ambapo watu wote wa Mungu wanapaswa “kushughulika kwa juhudi nyingi” na kujulisha habari njema kwa wengine. Mtume Paulo anatoa uhakikisho kwamba kazi hiyo ya jasho kwa kweli “si bure kuhusiana na Bwana.”—1 Kor. 15:58.