Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Okt. 15
“Ni nini kinachohitajiwa ili kutokeza ulimwengu ulio bora na wenye furaha zaidi? [Acha mtu ajibu.] Wanadamu wamejaribu aina moja ya serikali baada ya nyingine ili kufanya mambo yawe bora. Lakini ona maoni ya Mungu kuhusu jambo hilo. [Soma Yeremia 10:23.] Makala hii inafunua ‘Ufunguo kwa Ajili ya Ulimwengu Wenye Furaha,’ ikionyesha jinsi huo utakavyotokea karibuni.”
Amkeni! Okt. 22
“Je, unakubali kwamba leo watu wanaishi chini ya mkazo zaidi kuliko wakati mwingine wowote? [Acha mtu ajibu.] Biblia ilitabiri jambo hilo. [Soma 2 Timotheo 3:1.] Watu wengi huona maisha kuwa magumu sana hivi kwamba wao hukata tamaa. Gazeti hili linatoa kitia-moyo cha kweli. Linaonyesha jinsi ya kupiganisha kukata tamaa, na jinsi ya kufanya maisha yastahili kufurahiwa.”
MNARA WA MLINZI Nov. 1
Baada ya kutaja habari fulani yenye kushtua, uliza: “Kwa nini watu hufanya maovu kama hayo? Sisi sote tunajua lililo sawa na lililo kosa, lakini bado watu wanafanya mabaya. Kwa nini? [Baada ya kusikia jibu, soma Ufunuo 12:9.] Gazeti hili linaeleza jinsi ya kujikinga kwa kulinda dhamiri yetu.”
Amkeni! Nov. 8
“Labda utakubali kwamba tunaishi nyakati zenye jeuri. [Baada ya kusikia jibu, soma 2 Timotheo 3:3.] Mara nyingi, matendo ‘ya ukali’ hutukia hata katika familia. Makala hii, ‘Msaada kwa Wanawake Wanaopigwa,’ inatoa ujumbe wa tumaini. Huenda ukajua mtu fulani ambaye unaweza kushiriki ujumbe huo pamoja naye.”