Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/10/06
“Kwa kuwa Mungu anakaa mbinguni, watu wengi wanasema kwamba haiwezekani kabisa kumjua. Je, wewe pia umekwisha kuwazia hivyo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Yohana 17:3.] Gazeti hili linafasiria jinsi tunavyoweza kumjua Mungu.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Sisi wote tumekwisha kufiwa na wapendwa wetu. Je, unafikiri kwamba kuna mambo ambayo tunaweza kufanya ili kuwasaidia hata ikiwa wamekwisha kufa? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linatoa jibu la Biblia kuhusu ulizo hilo. Linazungumzia pia ahadi hii yenye kufariji.” Soma Yohana 5:28, 29. Kisha onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/11/06
“Leo, kuna mawazo mengi yenye kupingana kuhusu jinsi ya kulea watoto. Je, unafikiri kwamba wazazi wanaweza kupata shauri lenye kutumainiwa kuhusu jambo hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Zaburi 32:8.] Gazeti hili linaonyesha maagizo yenye kufaa kutoka katika Biblia kuhusu kulea watoto.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Je, umepata kujiuliza kwa nini kuna mateso mengi hivi ikiwa kuna Mungu mwenye upendo, mwenye haki na mwenye nguvu? [Acha mtu ajibu. Ona yale ambayo andiko hili linasema kuhusu mwenye kutuletea mateso. [Soma 1 Yohana 5:19.] Gazeti hili linafasiria kutokana na Biblia mambo ambayo Mungu anafanya ili kuondoa mateso.”