Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
MNARA WA MLINZI Okt. 15
“Maamuzi mengi tunayochukua yana uvutano wenye matokeo sana juu ya maisha yetu. Ni nini kinachoweza kutusaidia tuepuke kuchukua maamuzi yasiyo ya hekima? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mithali 3:6.] Toleo hili la Mnara wa Mlinzi linatoa miongozo mitano yenye kutegemea Biblia, inayoweza kutusaidia tuchukue maamuzi ya hekima.”
Amkeni! Okt. 22
“Je, umetambua kwamba zaidi na zaidi, tunasikia kuhusu vijidudu vinavyosababisha magonjwa ambavyo juu yavyo matunzo ya kiganga hayana matokeo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia sababu zinazotokeza jambo hilo na linapendekeza kile tunachoweza kufanya ili kujilinda. Linazungumzia pia ahadi ya Biblia kuhusu ulimwengu ambamo hakuna mtu yeyote atakayekuwa mgonjwa.” Soma Isaya 33:24.
MNARA WA MLINZI Nov. 1
“Wakati fulani, sisi sote tumepata kukatishwa tamaa na mtu fulani tuliyemtumainia. Je, umekwisha kujiuliza ikiwa kuna mtu yeyote unayeweza kumtumainia? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mithali 3:5.] Gazeti hili linaeleza kwa nini tunaweza kuweka tumaini letu lote katika Mungu. Linazungumzia pia jinsi tunavyoweza kutambua watu wanaostahili kutumainiwa.”
Amkeni! Nov. 8
“Vitu vinavyofanywa kwa petroli vinagusa karibu kila sehemu ya maisha yetu. Je, umekwisha kujiuliza jinsi maisha yangekuwa bila vitu hivyo? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi petroli ilivyokuja kutimiza fungu la maana sana katika jamii ya kisasa. Linaeleza pia kwa nini hatupaswi kuogopa kwamba siku moja petroli itamalizika kabisa.”