Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Watu fulani wanaamini kwamba kwa kadiri wanavyokuwa na fedha, hivyo wanakuwa na maisha yenye kutosheleza. Unafikiri kwamba ni kweli? [Acha mtu ajibu.] Ona yale aliyoandika mtu aliyekuwa tajiri sana. [Soma Mhubiri 5:10.] Gazeti hili linazungumzia maadili ya maana zaidi kuliko utajiri wa kimwili.”
Amkeni! Okt. 22
“Watu wengi wanaona kwamba ni jambo la maana kufundisha watoto tangu umri mdogo. Je, unaona kwamba jambo hilo linahitajiwa leo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Methali 22:6.] Toleo hili la Amkeni! linazungumzia mambo kamili ambayo wazazi wanaweza kufanya ili kusaidia watoto wao wakomae wakiwa watu wazima wanyofu na wenye kufanikiwa.”
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Watu wengi hawaamini kwamba viongozi wa kibinadamu wanao uwezo wa kutatua matatizo ya leo. Je, unafikiri kwamba kuna yeyote anayeweza kutimiza yale yanayotabiriwa katika mistari hii? [Soma Zaburi 72:7, 12, 16. Kisha acha mtu ajibu.] Gazeti hili linaeleza kiongozi huyu aliyetabiriwa ni nani na kile atakachotimiza.”
Amkeni! Nov. 8
“Watoto wanahitaji uongozi ili kupinga mikazo wanayopambana nayo leo; je, haukubaliani na hilo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waefeso 6:4.] Gazeti hili linazungumzia maana ya kweli ya nidhamu. Linazungumzia pia jinsi wazazi wanavyoweza kutoa uongozi na rekebisho bila kuvunja watoto wao moyo.”