Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 15/10/07
“Watu wengi wanafikiri kwamba hakuna uhakika kuhusu wakati ujao, wanasema kwamba ni vizuri zaidi kuishi kwa ajili ya leo tu. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu.] Yesu alisema maneno haya yenye kupendeza. [Soma Mathayo 6:34.] Gazeti hili linaeleza jinsi tunavyoweza kufanya mipango kwa ajili ya wakati ujao na wakati huohuo kuepuka kuuhangaikia kupita kiasi.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Sisi wote tumefiwa na wapendwa wetu. Je, unafikiri kwamba ni wenye kututazama wakiwa mbinguni? [Acha mtu ajibu.] Ona maneno ambayo Yesu alisema Lazaro alipokufa. [Soma Yohana 11:11.] Habari hii inaeleza ikiwa wafu wanaishi mahali fulani ao ikiwa ni wenye kulala wakingojea ufufuo.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 28.
Mnara wa Mlinzi 01/11/07
“Je, unafikiri kwamba ulimwengu ungekuwa mahali pazuri zaidi kuishi ikiwa watu wangejionyesha wanyenyekevu zaidi? [Acha mtu ajibu.] Ona jinsi Yesu alisema kuhusu sifa hiyo. [Soma Mathayo 23:12.] Habari hii inazungumzia umaana wa kuwa wanyenyekevu, hata katika ulimwengu huu ambamo watu ni wenye kushindana.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Zamani, watu walitafuta mara nyingi mwongozo katika Biblia. Lakini wengi wanasema kwamba wana mashaka sasa. Unafikiri nini? [Acha mtu ajibu. Kisha soma 2 Timotheo 3:16.] Amkeni! hii ya pekee inatoa maelezo yenye kuhakikisha kabisa kwamba Biblia iliongozwa na roho ya Mungu.”