Tuseme Nini Kuhusu Magazeti?
MNARA WA MLINZI Okt. 15
“Unawezaje kuwaeleza watoto na watu wengine kwa nini mambo mengi mabaya yanatukia leo? [Acha mtu ajibu.] Biblia inajibu ulizo, ‘Ni nani Husababisha Uovu Wote?’ [Soma 1 Yohana 5:19.] Makala hii ya Mnara wa Mlinzi itakusaidia uelewe yule mwovu ni nani na jinsi tunavyoweza kumpinga.”
Amkeni! Okt. 22
“Je, unafikiri kwamba sala za viongozi wa kidini au za mtu mwingine yeyote zinaweza kuleta amani duniani? [Acha mtu ajibu.] Biblia inaahidi wakati wa amani ya ulimwenguni pote. [Soma Isaya 9:6, 7.] Je, ulitambua kwamba mtawala wa pekee angeleta amani ulimwenguni? Makala hii ya Amkeni! inaonyesha yule mtawala ni nani na jinsi atakavyoleta amani ya kweli.”
MNARA WA MLINZI Nov. 1
“Wengi wetu hujaribu kuwa na uhusiano wenye amani pamoja na wengine. Lakini yaelekea utakubali kwamba mara nyingi hilo ni jambo gumu kufikia. [Acha mtu ajibu.] Biblia inaeleza kwa nini mambo ni hivyo. [Soma Yakobo 3:2.] Makala hii inaonyesha jinsi kuomba msamaha kunavyoweza kuwa ufunguo wa kurudisha na kudumisha amani.”
Amkeni! Nov. 8
“Unabii wa Biblia unaonyesha kwamba wakati unakuja ambapo hakuna mtu atakayesema, ‘Mimi ni mgonjwa.’ [Soma Isaya 33:24.] Je, hilo halitakuwa jambo la ajabu? [Acha mtu ajibu.] Hata hivyo, leo wanadamu wanataabishwa na magonjwa mengi, kutia ndani pigo la UKIMWI. Toleo hili la Amkeni! linajibu ulizo, Je, UKIMWI utakomeshwa wakati wowote?”