Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi Okt. 15
“Watu wengi wanaiona elimu kuwa siri ya kufanikiwa katika maisha. Je, unafikiri kwamba kuna aina ya elimu inayoweza kumsaidia mtu awe mtu bora na kumsaidia apambane na matatizo ya maisha? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Waroma 12:2.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kufaidika na elimu bora zaidi inayopatikana.”
Amkeni! Okt. 22
“Watu wengi wanafurahia kusoma gazeti fulani karibu kila siku. Je, unafikiri kwamba tunaweza kutegemea habari inayotolewa na magazeti? [Acha mtu ajibu.] Toleo hili la Amkeni! linatoa mapendekezo kuhusu jinsi ya kufaidika na usomaji wa gazeti. Linaonyesha pia kwa nini tunahitaji kuwa waangalifu.” Soma Methali 14:15.
Mnara wa Mlinzi Nov. 1
“Watu wengi ni wenye kutaabishwa na ukosefu wa haki katika ulimwengu. Je, unafikiri kwamba kuna yeyote anayeweza kabisa kubadili ulimwengu? [Acha mtu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia mambo yanayozuia mabadiliko. Linaonyesha pia ni nani atakayeondoa mambo hayo na jinsi atakavyoleta ulimwengu wenye amani ya kweli na usalama wa kweli.” Soma Zaburi 72:12-14.
Amkeni! Nov. 8
“Ulimwenguni pote kuna tofauti kubwa sana kati ya matajiri na maskini. Unafikiri kwamba kuna chochote kinachoweza kufanywa ili kuvunja tofauti hizo? [Acha mtu ajibu. Kisha soma Mathayo 6:9, 10.] Gazeti hili linaonyesha kwa nini tunaweza kuwa hakika kwamba Ufalme wa Mungu utaondoa tofauti hizo zinazolemea wanadamu leo.”