Programu Mpya ya Kusanyiko la Pekee la Siku Moja
1 Wakati vyombo vya habari na waelimishaji wa ulimwengu wanapotukuza utajiri wa kimwili, Neno la Mungu linatuhimiza ‘Tuwe Matajiri Katika Kazi Zilizo Bora.’ (1 Tim. 6:18) Hicho ndicho kichwa cha kusanyiko la pekee la siku moja kuanzia Septemba 2002. Ni kitia-moyo gani tutakachopokea kwenye kusanyiko hilo?
2 Mwangalizi wa mzunguko atazungumzia maana ya ‘Kuwa Matajiri Machoni pa Mungu,’ na atahoji ndugu fulani wanaojitahidi ili kujipatia utajiri wa kiroho. Katika hotuba yake ya kwanza, msemaji-mgeni ataonyesha jinsi watu wa Mungu wanavyotimiza “Kazi Zilizo Bora Wakati Huu wa Mavuno.” Kila mmoja wetu atatiwa moyo kufikiria jinsi tunavyoweza kushiriki kikamili zaidi katika kazi hiyo ya mavuno iliyoamriwa na Mungu na inayotimizwa leo.
3 Sisi ni wenye furaha kama nini tunapoona vijana Wakristo wakifuatia utajiri wa kiroho! Jambo hilo linamtukuza Yehova na linasaidia vijana kuweka msingi mzuri kwa ajili ya mapendeleo ya utumishi wakati ujao. Sehemu “Pongeza Vijana kwa Kazi Zilizo Bora za Kumtukuza Yehova” itakazia kazi zilizo bora ambazo vijana Wakristo wamekuwa wakizifanya katika mzunguko.
4 Kufuatia kazi zilizo bora kuna matokeo gani? Msemaji-mgeni atazungumzia jambo hilo katika hotuba yake ya mwisho, “Endelea Katika Kazi Zilizo Bora na Uvune Baraka za Yehova.” Atazungumzia sehemu nne ambazo katika hizo tunavuna baraka nyingi: (1) tukiwa watu mmoja mmoja, (2) tukiwa familia, (3) tukiwa kutaniko, na (4) tukiwa tengenezo la ulimwenguni pote.
5 Wale ambao wamejiweka wakfu kwa Yehova watapata nafasi ya kubatizwa. Ikiwa uko tayari kuchukua hatua hiyo, mjulishe mwangalizi-msimamizi mara moja.
6 Tarehe ya kusanyiko katika mzunguko wenu itakapotangazwa, fanya haraka kuchukua mipango kamili ili kuhudhuria. Jitahidi kufika mapema ili ushiriki wimbo na sala ya kufungua. Kuwapo na kusikiliza programu nzima ya kusanyiko la pekee la siku moja kutatutia nguvu ili tufuatie mwendo unaotufanya kweli kuwa matajiri machoni pa Mungu wetu, Yehova.