“Tulikweze Jina Lake Pamoja”
1 Mtunga-zaburi aliimba: “Mtukuzeni Yehova pamoja nami, Na tulikweze jina lake pamoja.” (Zab. 34:3) Mkusanyiko wetu wa Wilaya ujao wenye kichwa “Tembea na Mungu” utatutolea nafasi ya kulikweza au kulitukuza jina la Yehova pamoja na ndugu na dada zetu kutoka makutaniko mengi. Je, umefanya mipango kuhusu mahali pa kupanga, usafirishaji na kuhusu kuomba likizo kazini? Tutakuwa wenye hekima ikiwa tunashughulikia mambo hayo kimbele.—Met. 21:5.
2 Kufika Kwenye Mahali pa Mkusanyiko: Kuna mambo mengi ya kushughulikia tunapohudhuria mkusanyiko. Kuondoka nyumbani mapema kutatusaidia tuepuke kuchelewa kusikotazamiwa na kutatuwezesha kupata mahali pa kukaa pa wakati ili kushiriki kwa moyo wote katika wimbo na sala ya kufungua. (Zab. 69:30) Dakika chache kabla ya kuanza kipindi, mwenyekiti atakuwa mwenye kukaa jukwaani huku muziki wa Ufalme ukichezwa kuwa utangulizi. Sisi sote tunapaswa kuwa wenye kukaa wakati huo ili programu ipate kuanza kwa njia yenye utaratibu.—1 Kor. 14:33, 40.
3 Neno la Mungu linatuonya ‘tufanye mambo yetu yote yatendeke kwa upendo.’ (1 Kor. 16:14) Milango itakapofunguliwa pa saa 2:00 za asubuhi, kuwafikiria wengine kutatuzuia kukimbilia au kusukumana ili kupata mahali pa kukaa tunapopendelea. Viti vinaweza kuchungwa tu kwa ajili ya wale mnaosafiri nao katika gari moja au wale wanaoishi nanyi katika nyumba moja.—1 Kor. 13:5; Flp. 2:4.
4 Tafadhali tulete chakula cha mchana badala ya kutoka mahali pa mkusanyiko ili kununua chakula wakati wa mapumziko ya mchana-kati. Hilo litafanya wote kufurahia ushirika unaojenga na kuwa hapo mwanzoni, wakati kipindi cha kisha mchana-kati kinapoanza. Ikiwezekana, chombo kidogo cha kuchungia chakula au kinywaji kinachoweza kutiwa chini ya kiti chako kinaweza kutumiwa. Vyombo vikubwa zaidi vya kuchungia watu wengi chakula, kama vile familia kubwa inayokwenda kujitembeza; vyombo vinavyofanyizwa kwa bilauri; na vinywaji vyenye alkoholi haviruhusiwi mahali pa mkusanyiko.
5 Ili kuwasaida wale walio wazee na pia wale walio na ulemavu wa kimwili, mahali fulani patachungwa kwa ajili yao. Hilo litawafanya wawe wenye kukaa kwa ustarehe na kulindwa na mambo kama vile mvua na jua, ikiwa inawezekana. Tangazo kuhusu jambo hilo linapaswa kufanywa mwanzoni mwa kipindi cha kwanza.
6 Karamu ya Kiroho Inatungojea: Mfalme Yehoshafati ‘alitayarisha moyo wake kumtafuta Mungu wa kweli.’ (2 Nya. 19:3) Tunawezaje kutayarisha moyo wetu kabla ya mkusanyiko? Makala kwenye ukurasa wa mwisho katika matoleo ya Amkeni! ya Mei 22 na Juni 8 yanatoa mtazamo kimbele wa karamu ya kiroho itakayoandaliwa. Kwa nini usichukue wakati kufikiri juu ya makala hizo, ili kusitawisha hamu kwa ajili ya yale ambayo Yehova anatuwekea? Kutayarisha moyo wetu kunatia ndani pia kumwomba Yehova atusaidie kuelewa maana ya maagizo tutakayopata na kuyatumia.—Zab. 25:4, 5.
7 Sisi sote tunatamani kujifunza mengi zaidi kutoka Neno la Mungu, tukitambua kwamba kupitia hilo tunaweza kukua kufikia wokovu. (1 Pet. 2:2) Kwa hiyo, na tuhudhurie Mkusanyiko wa Wilaya “Tembea na Mungu” na hivyo ‘tulikweze jina la Yehova pamoja.’—Zab. 34:3.
[Maulizo ya Funzo]
1. Ni nafasi gani tutakayokuwa nayo ya kulikweza jina la Mungu pamoja, na ni nini tunaloweza kufanya sasa katika kujitayarisha?
2. Kwa nini ni jambo lenye faida kupanga kufika mapema mahali pa mkusanyiko?
3. Tunawezaje kuonyesha kwamba tunawafikiria wengine tunapotafuta mahali pa kukaa?
4. Ni nini mipango kuhusu mapumziko ya mchana-kati, na jinsi gani hilo ni lenye faida?
5. Ni mipango gani ambayo imechukuliwa kuhusu wale walio wazee na pia wale walio na ulemavu wa kimwili?
6. Tunawezaje kutayarisha mioyo yetu kwa ajili ya maagizo tutakayopokea?
7. Tamaa yetu ni nini, na kwa nini?
[Kisanduku Kwenye Ukurasa wa 3]
Njia za Kulikweza
Jina la Mungu
◼ Panga mambo kimbele
◼ Onyesha wengine upendo
◼ Tayarisha moyo wako