Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 8/04 uku. 1
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2005
  • Ujitayarishe Vizuri Ili Kufundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2004
km 8/04 uku. 1

Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo

Sehemu 2: Kujitayarisha ili Kuongoza Funzo

1 Kufundisha kwa matokeo kwenye funzo la Biblia kunahusisha mengi zaidi ya kuzungumzia tu habari na kusoma tu maandiko yaliyotajwa. Tunapaswa kutoa habari kwa namna inayogusa moyo wa mwanafunzi. Hilo linaomba kujitayarisha kabisa tukifikiria mahitaji ya mwanafunzi.—Met. 15:28.

2 Jinsi ya Kujitayarisha: Anza kwa kusali Yehova kuhusu mwanafunzi na mahitaji yake. Mwombe Yehova akusaidie kufikia moyo wa mwanafunzi. (Kol. 1:9, 10) Ili kuelewa kichwa waziwazi, chukua wakati wa kufikiria kichwa cha sura au somo, vichwa vidogo, na picha yoyote. Jiulize, ‘kusudi la kwanza la habari hii ni nini?’ Hilo litakusaidia kukazia mawazo makuu unapoongoza funzo.

3 Rudilia kwa makini habari fungu kwa fungu. Pata majibu ya maulizo yaliyochapishwa, ukitia alama tu juu ya maneno makuu na misemwa. Chunguza uone jinsi maandiko yanayotajwa yanavyohusiana na mambo makuu ya fungu, na uamue andiko la kusoma wakati wa funzo. Huenda utaona kuwa jambo lenye kusaidia kuandika maelezo mafupi kandokando kuhusu maandiko. Inafaa mwanafunzi atambue wazi kwamba yale anayojifunza yanatoka katika Neno la Mungu.—1 Tes. 2:13.

4 Patanisha Somo na Mahitaji ya Mwanafunzi: Kisha, chunguza somo ukifikiria hasa mahitaji ya mwanafunzi. Jaribu kufikiria kimbele maulizo yake na mambo ambayo yanaweza kuwa vigumu kwake kuelewa au kukubali. Jiulize: ‘Ni nini anachohitaji kuelewa au kuboresha ili kufanya maendeleo ya kiroho? Ninawezaje kufikia moyo wake?’ Kisha patanisha mafundisho yako na mambo hayo. Nyakati nyingine, huenda utaona uhitaji wa kutayarisha mfano fulani, maelezo fulani, au mfululizo wa maulizo ili kusaidia mwanafunzi kuelewa maana ya jambo au maandiko fulani. (Neh. 8:8) Epuka kuingiza habari za ziada ambazo hazihusiani sana na kichwa. Kujikumbusha kwa kifupi mwishoni mwa funzo kutamsaidia akumbuke mambo makuu.

5 Sisi ni wenye furaha kwelikweli wakati wapya wanapozaa matunda ya uadilifu kwa utukufu wa Yehova. (Flp. 1:11) Ili kuwasaidia wafikie mradi huo, jitayarishe vizuri kila wakati unapotaka kuongoza funzo la Biblia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine