Kisanduku Cha Maulizo
◼ Je, ni jambo lenye kufaa kubandika adresi yetu wenyewe ya Internete kwenye vitabu tunavyotolea watu?
Kwa kutumia cachet ao kwa kutumia kikaratasi kilichochapishwa, wahubiri fulani wamebandika adresi yao ya Internete kwenye magazeti ao kwenye trakti wanazotolea watu. Wale wenye kukubali vitabu wanaweza hivyo kuandikia mhubiri huyo ili wajulishwe habari za zaidi. Kujikaza huko ili kusaidia watu wenye kupendezwa kunaonyesha kwamba wahubiri hao wana nia njema. Hata hivyo, kituo cha Internete cha Mashahidi wa Yehova tayari kimeonyeshwa kwenye ukurasa wa mwisho wa magazeti na trakti. Kwa hiyo, si jambo lenye kufaa kubandika adresi yetu wenyewe ya Internete kwenye kitabu.
Mhubiri mwenyewe ataamua, zaidi sana anapokuja kurudilia watu katika eneo, ikiwa atawatolea kipande cha karatasi ambako anaandika adresi yake, bila kukibandika kwenye kitabu. Tunapaswa kuchukua hatua ya kurudilia wale wenye kupendezwa kuliko tu kuwaachia daraka la kutuandikia ili kupata habari zaidi. Kwa kumtembelea mtu, tunaweza kujua ikiwa anapendezwa kwelikweli tunapozungumza naye uso kwa uso.