Je, Tuko Tayari Kuhubiria Watu Wakati Hatukupanga Kufanya Hivyo?
1. Ni mfano gani unaoonyesha kwamba kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo kunaweza kuwa na matokeo mazuri?
1 Kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo kunaweza kuwa na matokeo mazuri sana. Biblia ina mifano mingi ya watu ambao walihubiria watu wakati hawakupanga kufanya hivyo. (Yoh. 4:7-15) Tunapaswa kufanya nini ili tujitayarishe kwa ajili ya aina hiyo ya mahubiri?
2. Namna gani kuvaa na kujipamba kwetu kunaweza kutusaidia kuwahubiria wengine?
2 Mvalio na Kujipamba: Kufikiria kwa uangalifu nyakati zote mvalio wetu na kujipamba kwetu kutatufanya tuwe tayari kuzungumzia wengine kuhusu imani yetu. (1 Tim. 2:9, 10) Ikiwa tunaona kwamba mvalio wetu na kujipamba kwetu hakumletee Yehova heshima, labda tutajizuia kuwahubiria wengine. Lakini ikiwa tunavaa na kujipamba kwa njia yenye kufaa, wengine watachochewa kutuuliza kwa nini tunavaa na kujipamba hivyo. Kwa mfano, walipokuwa wakisafiri, mume na muke wake ambao ni Mashahidi waliovaa kwa njia yenye kufaa walikaa pembeni ya mwanaume Mwislamu. Alipoona mvalio na kujipamba kwao, mwanaume huyo aliwauliza ikiwa wao ni Wakristo. Hilo liliongoza kwenye mazungumzo kuhusu Biblia, mazungumzo ambayo yalichukua saa 3.
3. Kwa kufuata mfano wa Yesu, namna gani umepata kuanzisha mazungumzo?
3 Jinsi ya Kuanzisha Mazungumzo: Yesu alipokutana na mwanamuke Msamaria kwenye kisima cha Yakobo, alianzisha mazungumzo kwa kumwomba tu maji ya kunywa. Sisi pia, tunaweza kuanzisha mazungumzo kwa kusema maneno machache ao kwa kuuliza tu ulizo. Hata ikiwa nyakati nyingine tunaweza kusita, kwa kutegemea msaada wa Yehova tunaweza ‘kujipa ujasiri’ ili kuanzisha mazungumzo.—1 The. 2:2.
4. Tunaweza kufanya nini ili tuwe tayari kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo?
4 Tutafute Nafasi: Wahubiri wengi wamepata nafasi za kuhubiria watu wakati hawakupanga kufanya hivyo. Tufikirie hali zetu, na tuone ni watu gani tunaoweza kukutana nao muda wa siku. Tuchukue vitabu vyenye kufaa na Biblia ndogo. Tuwe watazamaji, na tupendezwe na watu tunaokutana nao. Ikiwa tunafikiria mbele ya wakati nafasi tunazoweza kupata muda wa siku ili kuhubiria watu, labda tutakuwa tayari kuwatolea ushahidi kwa njia nzuri.—Flp. 1:12-14; 1 Pet. 3:15.
5. Kwa nini tunapaswa kuwa tayari kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo?
5 Tuna sababu mbili nzuri zinazotufanya tutumie nafasi tunazopata ili kuhubiria watu wakati hatukupanga kufanya hivyo—upendo kwa Mungu na kwa jirani. (Mt. 22:37-39) Kwa kuwa kazi ya kuhubiri inahitaji kufanywa kwa uharaka, tunapaswa kutia sehemu hii ya mahubiri katika programu yetu. Basi, tuwe tayari kutumia kila nafasi inayopatikana ili kuhubiria wengine habari njema ya Ufalme kunapokuwa kungali wakati.—Rom. 10:13, 14; 2 Tim. 4:2.