Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/10/09
“Watu wengi leo hawaamini tena kwamba kuna Muumba. Unafikiri ni kwa nini hivyo? [Acha mutu ajibu.] Andiko hili linaonyesha sababu moja. [Soma Habakuki 1:2, 3.] Habari hii inasaidia kujibu maulizo fulani ambayo watu wanajiuliza mara kwa mara kumhusu Mungu, maulizo ambayo yamewafanya waache kumwamini.” Onyesha habari inayoanzia kwenye ukurasa wa 11.
Amkeni! Mwezi wa 10
“Familia zinapatwa na matatizo mengi leo. Je, unakubaliana na jambo hilo? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi hawajui kwamba Biblia inatoa mashauri yanayofaa. Ona mfano mmoja. [Soma andiko moja katika gazeti.] Amkeni! hii ya pekee inaonyesha jinsi kanuni za Biblia zinavyoweza kusaidia watu wa familia mbalimbali washinde matatizo mengi.”
Mnara wa Mlinzi 01/11/09
“Je, unafikiri kwamba mambo yote yanayofundishwa katika makanisa yanatoka katika Biblia? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatuonya tuwe waangalifu ili tusidanganywe na mafundisho ya uongo. [Soma Wakolosai 2:8.] Gazeti hili linazungumzia aina sita ya mafundisho ambayo watu wameamini lakini ambayo hayapatane na Neno la Mungu.”
Amkeni! Mwezi wa 11
“Vyombo kama vile telefone na ordinatere vinatumiwa na watu wengi leo. Je, unafikiri kwamba vyombo vya teknolojia vinatusaidia tukomboe wakati ao vinatupotezea wakati? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanakubaliana na andiko hili linalotushauria tutumie wakati kwa hekima. [Soma Waefeso 5:15, 16.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunavyoweza kutumia vyombo vya teknolojia kwa hekima na kwa usawaziko.”