Tuseme Nini Kuhusu Magazeti
Mnara wa Mlinzi 01/09/10
“Nyakati nyingine watu wanafanya mambo mabaya kwa sababu ya kuongozwa vibaya na dini. Unafikiri kwa nini watu wanadanganywa hivyo? [Acha mutu ajibu.] Ona jinsi Biblia inatutia moyo. [Soma 1 Yohana 4:1.] Habari hii inazungumzia kwa nini ni jambo la maana kulinganisha mambo tunayoamini na yale ambayo Neno la Mungu linasema.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 10.
Amkeni! Mwezi wa 9
Soma Mathayo 5:39. Kisha useme: “Je, unafikiri Yesu alimaanisha kwamba tunapaswa kuteseka kimya-kimya tunapotendewa vibaya? [Acha mutu ajibu.] Habari hii inazungumzia kuhusu kujikinga na kutafuta ulinzi wa kisheria.” Onyesha habari iliyo kwenye ukurasa wa 10.
Mnara wa Mlinzi 01/10/10
“Watu wa dini za ulimwenguni pote wanasali. Je, unafikiri kwamba Mungu anasikiliza kabisa na kujibu sala hizo? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatutia moyo kusali. [Soma Wafilipi 4:6, 7.] Gazeti hili linatoa majibu ya Biblia kwa maulizo saba yanayoulizwa kwa ukawaida kuhusiana na sala.”
Amkeni! Mwezi wa 10
“Mara nyingi tunasikia kuhusu watu wanaodaganywa na wenzi wao wa ndoa, watu wa politike, na watu wengine. Je, unafikiri kwamba haiwezekani tena kupata watu waaminifu? [Acha mutu ajibu.] Watu wengi wanafikiri kwamba andiko hili ni lenye kutimia. Soma 2 Timotheo 3:1-5.] Gazeti hili linaeleza mahali ambapo unaweza bado kupata watu waaminifu.”