Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 6/12 uku. 1
  • Sababu 12 Zinazotufanya Tuendelee Kuhubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu 12 Zinazotufanya Tuendelee Kuhubiri
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Chukua kwa Uzito Kazi Yako ya Kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kazi Yetu ya Kuhubiri Inaonyesha Kwamba Tunampenda Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Uendelee Kuwa na Bidii Katika Kazi ya Kuhubiri
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Kazi ya Kuhubiri Inatufanya Tuendelee Kuwa Nguvu Kiroho
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 6/12 uku. 1

Sababu 12 Zinazotufanya Tuendelee Kuhubiri

Sababu gani tunahubiri na kufundisha habari njema? Je, kusudi letu kubwa ni la kuwasaidia watu wenye mioyo mizuri watembee kwenye barabara inayoongoza kwenye uzima? (Mt. 7:14) Hiyo ndiyo sababu ya kwanza kati ya sababu zilizo hapa chini, lakini hiyo si sababu yetu kubwa. Kati ya sababu 12 zilizo hapa chini, wewe unafikiri ni sababu gani iliyo ya maana zaidi inayotuchochea kuhubiri?

1. Kuhubiri kunasaidia kuokoa maisha.​—Yoh. 17:3.

2. Kuhubiri kunasaidia kuwaonya waovu.​—Eze. 3:18, 19.

3. Kuhubiri kunatimiza unabii wa Biblia.​—Mt. 24:14.

4. Kuhubiri kunaonyesha haki ya Mungu. Hakuna mutu atakayemulaumu Yehova kwa kusema kama hakuwatolea waovu nafasi ya kutubu mbele ya kuwaharibu.​—Mdo. 17:30, 31; 1 Tim. 2:3, 4.

5. Kuhubiri kunatufanya tulipe deni letu la kuwatolea watu walionunuliwa na damu ya Yesu musaada wa kiroho.​—Rom. 1:14, 15.

6. Kuhubiri kunatufanya tuepuke kuwa na deni ya damu ya watu.​—Mdo. 20:26, 27.

7. Kuhubiri ni jambo ambalo Mungu anatuomba kufanya ili tupate wokovu.​—Eze. 3:19; Rom. 10:9, 10.

8. Kuhubiri kunaonyesha kama tuna upendo kwa jirani.​—Mt. 22:39.

9. Kuhubiri kunaonyesha kama tunamutii Yehova na Mwana wake.​—Mt. 28:19, 20.

10. Kuhubiri ni sehemu ya ibada yetu.​—Ebr. 13:15.

11. Kuhubiri kunaonyesha kama tunamupenda Mungu.​—1 Yoh. 5:3.

12. Kuhubiri kunasaidia kufanya jina la Yehova litakaswe.​—Isa. 43:10-12; Mt. 6:9.

Bila shaka, kuna sababu zingine zinazotuchochea tuhubiri. Kwa mufano, wakati tunahubiri, imani yetu inatiwa nguvu na tunapata pendeleo la kufanya kazi pamoja na Mungu. (1 Kor. 3:9) Hata hivyo, sababu ya maana zaidi inayotuchochea kuhubiri ni ile ya 12. Iwe watu wanatusikiliza ao hapana, mahubiri yetu yanasaidia kufanya jina la Mungu litakaswe na kumufanya Yehova amujibu yule anayemuzihaki. (Met. 27:11) Kwa kweli, tuna sababu za lazima sana zinazotufanya ‘tuendelee kufundisha na kutangaza habari njema bila kuacha.’​—Mdo. 5:42.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine