Les jeunes s’interrogent... Que vais-je faire de ma vie ? (Sehemu ya 1)
Vijana wanapokomaa na kuwa watu wazima, wanapaswa kuchukua maamuzi ya maana. DVD yenye kichwa Les jeunes s’interrogent... Que vais-je faire de ma vie ? (Vijana Wanajiuliza—Namna Gani Nitatumia Maisha Yangu?) imetayarishwa ili kuwasaidia vijana wafanye maamuzi mazuri zaidi. Unapofungua DVD hiyo, kwenye menu principal, fungua kwenye neno Drame, kisha ona ikiwa unaweza kupata majibu kwa maulizo yaliyo katika fungu la 2. Kisha, rudi kwenye menu principal na ufungue kwenye neno Interviews na humo utaona neno Souvenirs, hapo unaweza kupata majibu ya maulizo yaliyo kwenye fungu la 3.
Drame: (1) Namna gani hali ya vijana wengi Wakristo leo inalingana na ile ya Timotheo anayezungumuziwa katika Maandiko ya Kigiriki ya Kikristo? (2) Namna gani André alikazwa sana ili awe muchezaji muzuri sana wa kukimbia? (3) Ndugu Fleissig alimuambia André nini kuhusu: (a) kujitoa kwa ajili ya Yehova na wakati uleule kujitoa kwa ajili ya michezo? (Mt. 6:24) (b) ni nini inayoweza kumupatia mutu furaha ya kweli? (c) jambo ambalo bakuli aliyotumia kwenye kambi ya mateso ilimukumbusha? (d) watu waliokuwa kwenye picha pamoja naye na bibi yake? (e) jambo la kwamba hakuhuzunika kwa kubadilisha miradi yake? (Flp. 3:8) (4) Namna gani kambo ao tate-mwanamuke wa André alijibia ulizo, “Ni vibaya mutu kuwa mukimbiaji mwenye kujulikana sana?” (Lu. 4:5-7) (5) Je, kushinda shindano la mbio kulimuletea André furaha ya kweli? (6) Ni jambo gani lenye kugusa moyo ambalo ulifurahia katika barua ambayo ndugu Fleissig alimuandikia André mbele ya kufa kwake? (Met. 10:22) (7) Ndugu Fleissig alimusaidia André kutambua nini?
Souvenirs (kukumbuka yale yaliyotokea katika maisha): (8) Ni kazi gani za kimwili ambazo ndugu na dada walifuatia, na sababu gani? (9) Je, walifikia yale waliyokuwa wakitafuta? (10) Ni jambo gani lililobadili kabisa maisha ya kila mumoja wao? (2 Kor. 5:15) (11) Ni sehemu gani za kazi ya Mungu zilizochukua nafasi ya kazi zao za zamani, na sababu gani walifikiri kwamba hawangeweza kufuatia kazi zote mbili mara moja? (12) Je, walikuwa na huzuni yoyote kwa sababu walibadili miradi yao katika maisha? (13) Ni mambo gani waliyosema ambayo yamefanya ufikirie namna unavyopaswa kutumia maisha yako?
Tafazali, utazame sehemu zingine za kuuliza watu maulizo na uwe tayari kutoa maelezo wakati wa mazungumuzo yatakayoendeshwa kwenye Mukutano wa Utumishi juma linalofuata.