‘Tuwe Wenye Kufanya Amani na Watu Wote’
1. Ni shauri gani la Biblia tunalopaswa kufuata tunapokutana na watu ambao wanachukizwa?
1 Sisi watu wa Yehova tunapenda amani, na huduma yetu ni ya amani. (Isa. 52:7) Lakini, wakati fulani tunakutana na watu ambao wanachukizwa kwa sababu tunawatembelea. Ni nini kitakachotusaidia tuwe wenye kufanya amani tunapokutana na hali kama hizo?—Rom. 12:18.
2. Sababu gani ni jambo la maana kuelewa hali ya wasikilizaji wetu?
2 Tuelewe Hali ya Wasikilizaji: Watu fulani wanachukizwa wakati tunawatembelea kwa sababu wanapinga kweli, lakini wengine wanaweza kuchukizwa kwa sababu ya mambo mengine yasiyohusiana hata na ujumbe wetu. Labda tuliwatembelea wakati usiofaa. Musikilizaji anaweza kuwa mwenye kukasirika kwa sababu ya matatizo aliyo nayo. Hata kama anakasirika kwa sababu ya habari njema, tusisahau kama anafanya hivyo kwa kuwa amedanganywa. (2 Kor. 4:4) Kuelewa hali ya musikilizaji kutatusaidia tutulie na kutambua kama hatukasirikie sisi.—Met. 19:11.
3. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamuheshimu musikilizaji?
3 Tuwe na Heshima: Watu wengi katika eneo wanashikilia sana imani yao. (2 Kor. 10:4) Wana haki ya kuamua ikiwa watatusikiliza ao hapana. Tusizarau hata kidogo mambo ambayo musikilizaji anaamini ao kumuonyesha kama yeye hajue kitu kwa sababu sisi tuna ujuzi mwingi wa Biblia kuliko yeye. Wakituomba tuondoke, basi tuondoke kwa heshima.
4. Tunaweza kuongea kwa upole namna gani?
4 Tuongee kwa Upole: Hata ikiwa wanatuambia maneno mabaya, tunapaswa kujibu kwa upole na kwa neema. (Kol. 4:6; 1 Pet. 2:23) Kuliko kuingia katika mabishano, jaribu kuzungumuzia jambo ambalo munakubaliana na musikilizaji wako. Labda kwa upole unaweza kumuuliza sababu gani anapinga ujumbe wako. Lakini, ili kuepuka kumukasirisha zaidi, wakati fulani ni vizuri zaidi kusimamisha mazungumuzo.—Met. 9:7; 17:14.
5. Tunapata faida gani ikiwa sisi ni wenye kufanya amani katika mahubiri?
5 Ikiwa sisi ni wenye kufanya amani, musikilizaji anaweza kukumbuka jambo hilo, na hivyo anaweza kumusikiliza Shahidi mwengine atakayemutembelea. (Rom. 12:20, 21) Hata ikiwa anaonekana kuwa mwenye kupinga ujumbe wetu sana, siku moja anaweza kuwa Shahidi. (Gal. 1:13, 14) Iwe musikilizaji anapendezwa na kweli ao hapana, tutamuheshimu Yehova na kupamba mafundisho yetu ikiwa tunabaki wenye kutulia na kuonyesha kwamba sisi ni wenye kufanya amani.—2 Kor. 6:3.