Tumia Magazeti ya Zamani
Kwa sababu magazeti ya zamani hayawezi kuwa yenye faida ikiwa yanawekwa ao yanatupwa, tunapashwa kujikaza kuyatolea watu. Gazeti moja tu linaweza kumuchochea mutu apendezwe na kweli na kumusukuma aanze kuliitia jina la Yehova. (Rom. 10:13, 14) Ona mapendekezo yanayoweza kutusaidia kutumia magazeti ya zamani.
Wakati unahubiri katika maeneo ambayo hayahubiriwe sana, bila kuonwa na watu, unaweza kuacha gazeti moja mahali ambapo hauwakute watu.
Wakati unahubiri mahali ambapo watu wanangojea, kwa mufano, kwa kungojea bus ao treni, uwaulize watu ikiwa unaweza kuwatolea kitu cha kusoma, uwaonyeshe magazeti mengi ya zamani, na uwaombe wachague.
Wakati unatembelea mahali watu wanafulia nguo kwa mashine, kwenye nyumba za kutunzia watu, kwenye hospitali, ao nafasi kama hizo katika eneo la kutaniko lenu, acha magazeti fulani ya zamani mahali ambapo watu wanangojea. Kwa kawaida, ni muzuri uombe ruhusa musimamizi wa mahali hapo ikiwa iko. Ikiwa unaona magazeti yameachwa hapo, ni muzuri zaidi usiache magazeti mengine.
Wakati unajitayarisha kuwarudilia watu, fikiria mambo yanayomupendeza kila mutu ambaye unapanga kutembelea. Ana familia? Anasafiri mara nyingi? Ni mulimaji? Chunguza magazeti ya zamani ili kuona ikiwa kuna habari ambayo atafurahia kusoma, na unaporudi, umuonyeshe habari hiyo.
Ikiwa unakutana nyumbani mutu aliyependezwa ambaye umetafuta kwa siku nyingi bila kumupata, umuonyeshe magazeti ya zamani ambayo hajapata.