“Tolea Watu Magazeti ya Zamani ao Broshua Yoyote Inayozungumzia Habari Zinazowapendeza”
Katika miezi ambamo tunatolea watu kitabu Biblia Inafundisha na kuwatolea funzo tunapowatembelea kwa mara ya kwanza, tunatiwa moyo ‘kumtolea mutu gazeti la zamani ao broshua yoyote inayozungumzia habari inayompendeza’ ikiwa ana kitabu hicho lakini hakubali funzo. Kwa nini?
Broshua na magazeti ya zamani yana habari tofauti-tofauti za wakati wetu zenye kufaa. Jambo fulani katika moja ya vichapo hivyo linaweza kugusa moyo wa msikilizaji wetu. Kwa hiyo, unapotia vichapo katika mfuko wako wa mahubiri, tia ndani broshua mbalimbali na magazeti ya zamani. Ikiwa hauna magazeti ya zamani, labda unaweza kuyapata kwenye Jumba la Ufalme. Kwa hiyo, ikiwa msikilizaji ana kitabu Biblia Inafundisha lakini hakubali funzo la Biblia, unaweza kumwonyesha magazeti fulani na broshua na kumwomba achukue yanayompendeza. Kisha, fanya mipango ya kumrudilia ili kuchochea kupendezwa kwake. Labda funzo la Biblia litaanzishwa.