“Sitamupata Tena Nyumbani!”
Umekwisha kusema maneno hayo juu ya mutu aliyependezwa? Hata kama umejikaza kumurudilia mutu huyo mara kwa mara, haujapata nafasi ya kutia maji mbegu uliyopanda. (1 Kor. 3:6) Wakati fulani, wahubiri wenye uzoefu wanaandikia mutu ambaye hawakukuta nyumbani barua, ao wanaandika ujumbe mufupi na kuuacha kwenye mulango. Ili kupambana na tatizo la kukosa mutu anayependezwa nyumbani, wahubiri fulani wanamuomba namba yake ya telefone, kwa mufano, kwa kumuuliza ikiwa ana telefone. Tunaweza kuripoti rudio wakati tunamurudilia mutu ao tunamuhubiri kupitia barua, tunamuandikia ujumbe kupitia Internete ao telefone, na pia wakati tunamuandikia ujumbe mufupi na kuuacha kwenye mulango wake ao tunamuita kwenye telefone. Hata kama ni vigumu kumupata nyumbani, tunaweza kuendelea kuchochea kupendezwa kwake.