MAISHA YA MUKRISTO
Tukomalishe Ufundi Wetu Wa Kuhubiri—Kuhubiri Kupitia Telefone
JUU YA NINI NI LAZIMA KUFANYA VILE: Kuhubiri kupitia telefone ni njia ya maana ya “kutoa ushahidi kamili juu ya habari njema.” (Mdo 20:24)a Kunatusaidia kuhubiria mutu hata kama haiwezekane tuonane naye uso kwa uso.
NAMNA YA KUFANYA VILE:
Ujitayarishe. Chagua habari yenye kufaa. Kisha panga muzuri mambo yenye unapenda kusema ao uiandike. Unaweza pia kutayarisha ujumbe mufupi wenye kuonyesha juu ya nini uliita, kama unapata jibu ya mashini ya kujibia telefone. Ni muzuri kukaa ku meza ukiwa na karatasi yako kwenye uliandika mambo yenye utatumia, unaweza hata kufungua JW Library® ao jw.org® ku chombo chako cha kielektroniki.
Ukuwe mwenye kutulia. Sema tu vile unasemaka. Unaweza kucheka na kufanya ishara vile tu unafanyaka mbele ya mutu fulani. Epuka kusema kwa kukata-kata maneno. Ni muzuri kuhubiri na wengine. Kama musikilizaji anauliza ulizo, uirudilie kwa sauti juu mwenye uko unahubiri naye asikie, pengine anaweza kukusadia upate jibu
Sema habari yenye mutazungumuzia siku ingine. Kama mutu anapendezwa, unaweza kumuachia ulizo yenye utajibia siku yenye utamuita tena. Unaweza kumuandikia ao kuenda kumupatia kichapo ao kumutumia kichapo kupitia chombo cha kielektroniki. Ao unaweza kumutumia moja ya video zetu ao habari ingine kutoka mu vichapo. Kama inawezekana, umuonyeshe kuhusu Masomo ya Biblia ku Enternete ao juu ya habari ingine yenye kuwa ku site yetu.
a Kama kuhubiri kwa kutumia telefone kunakubaliwa mu inchi yenu, munapaswa kufanya vile kwa kuheshimia sheria ya inchi yenu.