Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/01/15
“Inaonekana rushwa imekuwa tatizo katika serikali. Unawaza ni kwa sababu gani? [Acha mutu ajibu.] Ona wazo hili la Biblia ambalo lilinivutia. [Soma Mhubiri 7:20.] Gazeti hili linatoa mawazo ya Biblia kuhusu namna Mungu atamaliza rushwa. Nakuomba uchukue wakati kidogo wa kulisoma. Kamata gazeti lako.”
Amuka! Mwezi wa 1
“Watu wengi wanaamini kwamba uzima ulitokana na mageuzi, lakini wengine hawako hakika kabisa. Weye unawaza uzima ulianza namna gani? [Acha mutu ajibu.] Miaka mingi ya uchunguzi inaonyesha kwamba uzima unatokana na uzima mwengine. Hilo linapatana na maneno haya ya Biblia. [Soma Zaburi 36:9.] Gazeti hili linaonyesha kwamba watu wengi wamefikia kutambua kama uzima una mambo mengi na ni wenye kushangaza sana, kwa hiyo, hauwezi kutokana na mageuzi.”