Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/08
“Tunatembelea kwa muda mufupi majirani wetu ili kuwaonyesha namna wanaweza kupambana na tatizo moja lenye linawapata watu wote. Utakubaliana na miye kwamba jambo moja lenye linatuumiza zaidi ni kifo cha mutu mwenye tunapenda, sivyo? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatutia moyo kwa kutupatia ahadi hii. [Soma Ufunuo 21:3, 4.] Biblia inatupatia tumaini kwamba wapendwa wetu wenye wamekwisha kufa watafufuliwa. Gazeti hili linaonyesha namna jambo hilo litafanyika.”
Amuka Mwezi wa 8
“Tunatembelea majirani wetu ili kuwatolea gazeti lenye kuonyesha ni kiasi gani cha habari kiko katika chembe za mwili wetu. [Onyesha jalada la gazeti Amuka!] Watu wengi hawaamini kwamba uzima uliumbwa, na wengine wanaamini kwamba uliumbwa. Weye unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linazungumuzia mambo yenye imevumbuliwa juu ya chembe za mwili, na mambo hayo inaonyesha kwamba mwili uko na chembe nyingi sana; hilo limewashangaza wanasayansi fulani na kuwafanya wajiulize ikiwa kabisa hakuna Muumbaji.”