Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Munara wa Mulinzi 01/10
“Tunatolea kila mutu katika eneo hili gazeti Munara wa Mulinzi lenye kupendeza sana. [Umuonyeshe ukurasa wa kwanza wa gazeti.] Watu fulani wanawaza kama kusali ni kupoteza wakati kwa sababu hakuna mutu mwenye anasikiliza sala. Wengine wanaamini kwamba Mungu anasikiliza sala zao. Weye, unawaza nini? [Acha mutu ajibu.] Ona jambo lenye Biblia inasema juu ya sala. [Soma Isaya 30:19.] Gazeti hili linasadikisha kwamba Mungu anasikia na anajibu sala zenye zinatolewa kulingana na mapenzi yake.”
Amuka Mwezi wa 10
“Tunatembelea watu kwa muda mufupi katika eneo hili kwa sababu watu wengi wanajiuliza sababu gani Mungu anaacha watu wateseke. Unawaza kuuliza Mungu ulizo kama hili ni kukosa imani? [Acha mutu ajibu.] Ayubu, mwanaume mwaminifu, alitaka kuuliza Mungu ulizo moja. [Soma Ayubu 23:3-5.] Gazeti hili linazungumuzia maulizo matatu yenye watu wangetaka wamuulize Mungu kama wangepewa nafasi ya kufanya hivyo, na linaleta majibu ya Biblia yenye kusadikisha.”