Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Mwezi wa 9 uku. 8
  • Epuka Mitego Hii Wakati Unaongoza Funzo la Biblia

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Epuka Mitego Hii Wakati Unaongoza Funzo la Biblia
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Saidia Mwanafunzi Wako wa Biblia Afikie Kubatizwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
  • Kufundisha mu Njia ya Mwepesi
    Penda Watu—Juu Ufanye Wanafunzi
  • Jinsi Ya Kufanya Wanafunzi Kwa Msaada Wa Kitabu Ujuzi
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Kuongoza Mafunzo ya Biblia Yenye Maendeleo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2004
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
mwb16 Mwezi wa 9 uku. 8

MAISHA YA MUKRISTO

Epuka Mitego Hii Wakati Unaongoza Funzo la Biblia

Maandishi
Ndugu anasema mingi wakati anajifunza na mwanafunzi wake

Kusema Mingi: Haiko lazima ufasirie kila jambo. Yesu alitumia maulizo ili kusaidia watu wafikiri na wafikie kupata jibu. (Mt 17:24-27) Maulizo yanafanya funzo lichangamuke na yanakusaidia kujua mambo yenye mwanafunzi anaelewa na kuamini. (be uku. 253 fu. 3-4) Wakati unauliza ulizo, ngojea jibu. Kama mwanafunzi hajibie muzuri, kuliko kumuambia jibu, tumia maulizo yenye yatamusaidia afikie kupata jibu. (be uku. 238 fu. 1-2) Zungumuza kwa mwendo wenye utasaidia mwanafunzi aelewe mambo mapya.—be uku. 230 fu. 4.

Maelezo mengi yenye kuchangana-changana juu ya sababu gani tunazeeka

Kuchanga-changa mambo: Epuka kueleza mambo yote yenye unajua juu ya habari yenye munajifunza. (Yoh 16:12) Kazia wazo kubwa lenye kuwa katika fungo. (be uku. 226 fu. 4-5) Maelezo mengi, hata kama ni yenye kufurahisha, yanaweza kufanya wazo kubwa lisionekane wazi. (be uku. 235 fu. 3) Kama mwanafunzi anaelewa wazo kubwa, muende kwenye fungo lenye kufuata.

Ndugu anazungumuzia mambo mengi sana na anavuruga mwanafunzi

Kujifunza Mambo Mengi: Kusudi letu ni kugusa moyo wa mwanafunzi, haiko kutafuta kumaliza kitabu. (Lu 24:32) Tumia nguvu ya Neno la Mungu kwa kukazia maandiko ya maana ya habari yenye munajifunza. (2Kor 10:4; Ebr 4:12; be uku. 144 fu. 1-3) Tumia mifano yenye kueleweka. (be uku. 245 fu. 2-4) Tambua magumu ya mwanafunzi wako na mambo yenye anaamini, na upatanishe funzo kulingana na hali yake. Umuulize maulizo kama haya: “Unawaza nini juu ya mambo yenye unajifunza hapa?” “Mambo haya yanatufundisha nini juu ya Yehova?” “Unawaza utapata faida gani kama unatumikisha mashauri haya?”—be uku. 238 fu. 3-5; uku. 259 fu. 1.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine