Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwb16 Mwezi wa 11 uku. 5
  • Namna ya Kutumia Kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kutumia Kitabu Biblia Inatufundisha Nini?
  • Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Fuata Mfano wa Mwalimu Mkuu Unapotumia Kitabu Biblia Inafundisha
    Huduma Yetu ya Ufalme—2007
  • Biblia Inafundisha— Kitabu Chetu cha Lazima cha Kujifunzia Biblia
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
  • Kisanduku cha Maulizo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2008
  • Furahia Funzo Letu la Kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2006
Ona Habari Zaidi
Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2016
mwb16 Mwezi wa 11 uku. 5

MAISHA YA MUKRISTO

Namna ya Kutumia Kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

Biblia Inatufundisha Nini?

Kitabu Biblia Inatufundisha Nini? na kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? vinafanana. Vyombo hivyo viwili vya kufundishia viko na kweli zilezile na habari zinafuatana kwa namna moja. Lakini, kitabu Biblia Inatufundisha Nini? kinatumia maneno mepesi na kwa njia yenye kueleweka wazi zaidi. Kimetayarishwa kwa ajili ya wale wanaweza kuwa na magumu ya kuelewa kitabu Biblia Inafundisha. Kitabu Biblia Inatufundisha Nini? hakina nyongeza, lakini pa nafasi ya nyongeza kuna maelezo yenye inafasiria maneno magumu yenye kutumiwa katika kitabu. Sura hazina maulizo ya utangulizi ao kisanduku cha maulizo ya kurudilia. Lakini, zinamalizia kwa kueleza kwa kifupi kweli za Biblia zenye zilifasiriwa katika habari. Kama vile kitabu Biblia Inafundisha, tunaweza kuachia watu kitabu Biblia Inatufundisha Nini? wakati wowote, hata kama haiko toleo la mwezi. Namna gani tunaweza kutumia kitabu Biblia Inatufundisha Nini? wakati tunaongoza funzo la Biblia?

Kifupi cha sura katika kitabu Biblia Inaweza Kutufundisha Nini?

KIFUPI CHA SURA: Watu wengi wanapenda namna yetu ya kuongoza funzo la Biblia, ni kusema, kusoma fungu katika kitabu Biblia Inafundisha kisha kuuliza ulizo. Lakini, wakati fulani inawezekana mwanafunzi wako hajue luga ao hajue kusoma muzuri. Katika hali hiyo, unaweza kuchagua kutumia kitabu Biblia Inatufundisha Nini?. Kisha, unaweza kutumia kifupi cha sura kwa ajili ya funzo na unaweza kumuomba mwanafunzi ajisomee habari. Kila kweli ya Biblia inaweza kufundishwa kwa dakika 15 hivi. Kwa sababu kifupi cha sura hakina mambo yenye kuwa katika habari kubwa, mwalimu anapaswa kujitayarisha muzuri, kwa kufikiria mahitaji ya mwanafunzi. Kama mwalimu anaongoza funzo katika habari kubwa, kifupi cha sura kinaweza kutumiwa ili kujikumbusha.

Maelezo kwenye mwisho wa kitabu Biblia Inatufundisha Nini?

MAELEZO KWENYE MWISHO WA KITABU: Maneno na habari zenye kuwa kwenye mwisho wa kitabu zinapangwa namna zinafuatana katika kitabu. Mwalimu anaweza kuamua ikiwa watazungumuzia maelezo yenye kuwa kwenye mwisho wa kitabu Biblia Inatufundisha Nini? wakati wa funzo.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine