Mikusanyiko Yetu ya Wilaya—Inashuhudia Kabisa Kweli
1. Sikukuu za kawaida za kila mwaka ziliwatolea Waisraeli nafasi ya kutafakari na kuzungumuza juu ya mambo gani ya lazima?
1 Waisraeli walikusanyika mara tatu kwa mwaka kwa ajili ya sikukuu za kawaida. Hata ikiwa ni wanaume tu ndio waliombwa kuhuzuria sikukuu hizo, mara nyingi familia nzima zilienda Yerusalemu ili kufurahia mikusanyiko hiyo. (Kum. 16:15, 16) Mikusanyiko hiyo iliwatolea nafasi ya kutafakari ao kufikiri sana, na kuzungumuzia mambo ya kiroho. Kwa mufano, walizungumuzia kwamba Yehova ni mukarimu na mutoaji mwenye upendo. (Kum. 15:4, 5) Tena, walizungumuzia kwamba walipaswa kutegemea uongozi na ulinzi wake. (Kum. 32:9, 10) Waisraeli wangeweza pia kutafakari juu ya jambo la kwamba wao ni taifa linaloitwa kwa jina la Mungu, kwa hiyo wanapaswa kuonyesha njia zake za haki katika maisha yao. (Kum. 7:6, 11) Leo pia, tunafaidika na mikusanyiko ya wilaya tunayofanya kila mwaka.
2. Namna gani programu ya mukusanyiko wa wilaya inatusaidia kuelewa vizuri kweli ya Biblia?
2 Programu Inayotusaidia Kuelewa vizuri Kweli: Kwenye mikusanyiko yetu ya wilaya, tunafuata hotuba, drama, maonyesho, na sehemu za kuuliza maulizo. Sehemu hizo zinatusaidia kuelewa vizuri kweli ya Biblia na namna ya kuitumia katika maisha yetu. (Yoh. 17:17) Tayari kazi nyingi zinafanywa ili kutayarisha mukusanyiko wa wilaya wa mwaka huu. Tengenezo la Yehova linatayarisha programu ambayo inatosheleza hasa mahitaji ya kiroho ya watu duniani pote. (Mt. 24:45-47) Je, unangojea kwa hamu ili kufuata na kusikiliza mambo yatakayozungumuziwa kwenye mukusanyiko wetu wa wilaya?
3. Tunapaswa kufanya nini ili tufaidike na programu?
3 Bila shaka, tutafaidika sana na programu hiyo ikiwa tutahuzuria siku zote tatu na kufuata programu kwa uangalifu. Umujulishe bwana wako wa kazi kwamba utachukua siku za mapumuziko wakati huo. Siku hizo tatu uwe unapumuzika vya kutosha kila usiku ili usisinzie wakati wa programu. Ndugu na dada wengi wametambua kama kumutazama musemaji na kuandika mambo machache yanawasaidia wafuate programu kwa uangalifu. Usiruhusu telefone yako ikukengeushe ao kuwasumbua wengine. Epuka kuzungumuza-zungumuza, kuandika-andika ujumbe kwa njia ya telephone ao kukula wakati wa programu.
4. Namna gani wazazi wanaweza kuwasaidia watoto wao wafaidike na mukusanyiko?
4 Wakati wa sikukuu ya miaka ya Sabato, wakati familia za Israeli zilikusanyika ili kusikiliza usomaji wa Sheria wakati wa Sikukuu za Vibanda, walikuwa na ‘watoto wao wadogo’ “ili wasikilize na ili wajifunze.” (Kum. 31:12) Inatia moyo kabisa kuona watu wa familia wanakaa pamoja wakati wa mukusanyiko na kuwaona watoto wanafuata programu kwa uangalifu bila kusinzia! Kila mangaribi, munaweza kuchunguza mambo muliyoandika na kuzungumuzia pamoja mambo ambayo mulifurahia kwenye mukusanyiko siku hiyo. ‘Ujinga umefungwa pamoja na moyo wa mutoto,’ kwa hiyo wazazi wanapaswa kuwalinda watoto wao, kutia ndani vijana, wakati wa mapumuziko, kuliko ‘kuwaachilia.’—Met. 22:15; 29:15.
5. Namna gani mwenendo wetu muzuri unaipamba kweli?
5 Mwenendo Wetu: Tunapokuwa kwenye mukusanyiko, mwenendo wetu muzuri unaipamba kweli. (Tito 2:10) Wapolisi na watu wengine wenye mamlaka wanatambua wakati watu wa kikundi fulani wanafuata kanuni za Kikristo na kuonyesha kila mutu wema na uvumilivu. (Kol. 4:6) Mwaka uliopita musimamizi wa michezo na mambo ya kujiburudisha katika muji ambamo mukusanyiko wa wilaya ulifanywa aliandikia Halmashauri ya mukusanyiko hivi: “Nataka kuwapongeza kwa sababu ya adabu na usafi wa waamini wenu wakati wa mukusanyiko.”
6. Namna gani muvalio wetu unaweza kuipamba kweli?
6 Tunapovaa kadi ya utambulisho tunaonyesha kwamba tuna mukusanyiko na tunawasaidia wengine mashahidi watujue, lakini pia tunawatolea wale wanaotutazama ushahidi. Watu katika muji wataona kama wale wanaovaa kadi ya utambulisho wanavalia vizuri na kwa kiasi, hawavalie manguo ya ovyoovyo na yanayoamusha tamaa mbaya; mivalio ambayo inaenea ulimwenguni leo. (1 Tim. 2:9, 10) Kwa hiyo, tunapaswa kufikiria namna tunavyovalia na kujipamba tunapokuwa katika muji wa mukusanyiko. Kuja kwenye mukusanyiko ukiwa mwenye kuvaa kapitula ao mupira, ni kukosa adabu. Hata ikiwa mukusanyiko utafanywa katika uwanja ulio wazi, tunapaswa kuvalia kwa heshima. Ikiwa tunabadili mavazi kisha programu na kwenda kwenye restora, tusisahau kama tunapaswa kuonyesha mwenendo safi wakati wote wa mukusanyiko na kuepuka kuvalia ovyoovyo.
7. Namna gani tunaweza kufurahia umoja wetu wa Kikristo wakati wa mukusanyiko?
7 Kwenye sikukuu za kawaida, Waisraeli walifurahia kukutana pamoja na waabudu wenzao kutoka sehemu zingine ili kutiana moyo, na hilo liliwasaidia kuwa na umoja. (Mdo. 2:1, 5) Mikusanyiko yetu ya wilaya inatutolea nafasi ya kuonyesha kabisa kwa njia ya pekee upendo wetu wa kindugu. Mara nyingi sehemu hiyo yenye kufurahisha ya paradiso yetu ya kiroho inawashangaza wale wanaotutazama. (Zab. 133:1) Kuliko kutoka katika uanja wa mukusanyiko wakati wa mapumuziko ili kununua chakula, ni vizuri zaidi kuleta chakula chepesi tutakachokula, na kufaidika na nafasi hizo ili kukutana na kuzungumuza na ndugu na dada wanaokaa karibu nasi!
8. Tuna sababu gani za kujitolea ili kutumikia kwenye mukusanyiko ikiwa hali zetu zinaruhusu?
8 Wale wanaotutazama wanashangazwa na utaratibu ulio kwenye mukusanyiko, zaidi sana wanaposikia kwamba kazi inafanywa na watu wenye kujipendea. Je, unaweza ‘kujitolea kwa kujipendea’ ili kutumikia kwenye mukusanyiko? (Zab. 110:3) Mara nyingi familia nzima zinatumika ili kuwazoeza watoto wao wawe na roho ya kujitolea. Ikiwa wewe ni mutu mwenye haya, kutumika kwenye mukusanyiko ni nafasi nzuri ya kujuana na wahuzuriaji wengine. Dada mumoja alisema hivi: “Kutosha familia yangu na marafiki wachache, sikujua watu wengi huko. Lakini niliposaidia kufanya kazi ya usafi, nilijuana na ndugu na dada wengi. Nilifurahi sana!” Kufanya kazi kwenye mukusanyiko kutakuongezea marafiki katika maisha na jambo hilo litakuletea furaha nyingi. (2 Kor. 6:12, 13) Ikiwa haujajitolea kutumikia kwenye mukusanyiko, omba wazee wakuambie jambo unaloweza kufanya ili wewe pia usaidie.
9. Namna gani tutawaalika wengine ili wahuzurie mukusanyiko?
9 Tuwaalike Wengine: Kama tulivyofanya miaka iliyopita, mwaka huu pia majuma matatu mbele ya mukusanyiko wetu kuanza, tutafanya kampanye ya kuwaalika wengine. Makutaniko yatajikaza kuwatolea watu wengi kadiri iwezekanavyo mialiko hiyo katika eneo lao. (Soma kisanduku “Namna ya Kumutolea Mutu Mwaliko”) Mialiko itakayobaki kisha kampanye itapelekwa kwenye mukusanyiko. Wahuzuriaji watatumia mialiko hiyo watakapotoa ushahidi wanapoenda ao wanapotoka kwenye mukusanyiko katika muji wa mukusanyiko.
10. Eleza mambo yaliyotokea yanayoonyesha kama kampanye tunayofanya kila mwaka ili kuwaalika watu kwenye mukusanyiko inazaa matunda.
10 Je, wale tunaogawia mialiko wanafika kwenye mukusanyiko? Kwenye mukusanyiko moja, ndugu aliyetumika kwenye kazi ya ukaribishaji alisaidia bwana moja na bibi yake kupata nafasi ya kukaa. Watu hao walimuambia kama walipokea mwaliko na “waliuona kuwa wenye kupendeza.” Walisafiri kilometa zaidi ya 320 ili kuhuzuria mukusanyiko huo! Mufano mwengine, dada moja alikuwa akihubiri nyumba kwa nyumba, alimutolea mwaliko mwanaume moja ambaye alionekana kuwa anataka kujua vile mukusanyiko huo utakuwa. Kwa hiyo dada yetu alichukua wakati wa kuzungumuza naye juu ya mwaliko huo. Siku fulani baadaye, dada alimuona mwanaume huyo na rafiki yake kwenye mukusanyiko wakiwa na kichapo kilichotolewa kwenye mukusanyiko!
11. Sababu gani ni jambo la maana kuhuzuria mikusanyiko ya wilaya?
11 Sikukuu za kawaida ambazo Waisraeli walikuwa wakifanya kila mwaka zilionyesha upendo wa Yehova ili kuwasaidia ‘wamutumikie kwa njia isiyo na kosa na katika kweli.’ (Yos. 24:14) Vivyo hivyo, tunapohuzuria mikusanyiko yetu ya wilaya inayofanywa kila mwaka, hilo linatusaidia “tuendelee kutembea katika kweli” na hiyo ni sehemu ya maana ya ibada yetu. (3 Yoh 3) Yehova na abariki jitihada za wote wanaopenda kweli ili kuhuzuria na kufaidika kabisa na mukusanyiko!
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 4]
Tunapokuwa kwenye mukusanyiko, mwenendo wetu muzuri unaipamba kweli
[Wazo la fungu kwenye ukurasa 5]
Majuma matatu mbele ya mukusanyiko wetu kuanza, tutafanya kampanye ya kuwaalika wengine
[Sanduku katika ukurasa wa 3-6]
Mukusanyiko wa Wilaya 2012—Mambo ya Kukumbuka
◼ Saa: Siku zote tatu programu itaanza pa saa 2:20 (8h20) asubuhi. Lakini, katika miji mikubwa ifuatayo: Brazzaville, Goma, Kananga, Kikwit, Kinshasa, Kisangani, Kolwezi, Likasi, Lodja, Lubumbashi, Matadi, Mbandaka, Mbuji-Mayi, Mwene Ditu, Pointe Noire na Tshikapa, programu itaanza kila siku asubuhi pa saa 3:20 (9h20). Milango itafunguliwa asubuhi pa saa 1:00 (7h00) ao saa 2:00 (8h00), kulingana na mahali. Wakati muziki wa kufungua utakapoanza, sisi wote tunapaswa kukaa ili programu iweze kuanza kwa utaratibu. Siku ya Tano na Siku ya Posho programu itamalizika mangaribi pa saa 9:55 (15h55) na Siku ya Yenga itamalizika pa saa 8:20 (14h40).
◼ Kuchungia Wengine Viti: Munaweza kuchungia viti wale tu munaoishi nao, wale munaosafiri nao katika motokari moja ao wale munaojifunza pamoja nao Biblia kwa sasa.—1 Kor. 13:5.
◼ Chakula cha Midi: Inapendekezwa kwamba kila mutu alete kitu fulani cha kula kisicho kizito lakini cha kujenga mwili, kwa mufano: mikate ao keki, matunda, kalanga, vitumbua ao ndazi. Vinywaji kama vile maji, kahawa ao chai vinapaswa kutiwa katika vyombo visivyoweza kuvunjika ili kuepuka aksida. Hairuhusiwi kuleta pombe kwenye mukusanyiko. Ikiwa tunaleta chakula na kinywaji chetu, hatutahitaji kununua vyakula kwa wale wanaouzisha chakula inje. Kuepuka kununua vyakula kwa wauzishaji hao kunasaidia kuonyesha kama sisi ni watu safi. (Tafazali, Mujue kama wale wanaouzisha chakula inje hawaruhusiwi kuingia katika eneo la mukusanyiko wakati wowote.—Yoh 2:13-17.)
◼ Usafi: Imeonekana mara nyingi kama wale wanaonunua vyakula inje wanatupa chini makaratasi ao masashe. Hivyo, eneo lote linajaa makaratasi, vifuko vya plastiki, masashe, machupa ya plastiki ua vinywaji-sukari, na kazalika. Ikiwa mutu anaamua kununua chakula inje (kwa mufano: bonbons, biskwiti, ndazi ao vitumbua, vipande vya samaki ao chakula kingine) anapaswa kutupa makaratasi ya kufungia vyakula katika chombo cha kutupia uchafu kuliko kutupa chini. Tukiona mutu fulani ametupa kipande cha karatasi ao cha plastiki chini, tunapaswa kukiokota na kukitia katika chombo cha kutupia uchafu. Tafazali, tujikaze sana ili kulinda mahali petu pa mukusanyiko na eneo la kandokando vikiwa safi. Kila mutu anayehuzuria anapaswa kuhangaikia usafi. Ikiwa kila mutu anatimiza sehemu yake, mwishoni mwa kila siku, mahali pa mukusanyiko pataachwa pakiwa safi. Tunapenda kuonyesha katika maisha yetu sifa za Mungu mutakatifu ambaye tunaabudu.—1 Pet. 1:15, 16; Kut. 19:10; Kum. 23:14.
◼ Michango: Tunaweza kuonyesha shukrani yetu kwa ajili ya mipango ya mukusanyiko kwa kutoa michango ya kujipendea mahali pa mukusanyiko, ili kutegemeza kazi ya duniani pote. Sheke zote zinazotolewa kwenye mukusanyiko zinapaswa kuandikwa kwa jina “ Association ‘ Les Témoins de Jéhovah. ’ ”
◼ Aksida na Mambo Yanayoomba Kutenda kwa Haraka: Ikiwa kunatokea jambo linaloomba kutenda kwa haraka kwenye mukusanyiko, tafazali unaweza kumuelezea ndugu mukaribishaji aliye karibu ambaye bila kuchelewa atajulisha ndugu wanaoshugulika na Matunzo ya Haraka ili waamue ikiwa hali inaomba kutoa musaada unaohitajiwa.
◼ Dawa: Ikiwa unatumia dawa ulizoagizwa na daktari, tafazali usisahau kubeba dawa zako kwa kuwa hazitapatikana kwenye mukusanyiko. Kwa kuwa shindano za wale wanaogonjwa diabete ni zenye hatari, zinapaswa kutupwa mahali panapofaa; hazipaswi kutupwa katika chombo cha kutupia uchafu kwenye mukusanyiko.
◼ Kukamata Picha: Ukikamata picha kwenye mukusanyiko wakati wa kipindi, tafazali usitumie mwangaza (flash). Tafazali, usiwaite mahali pa mukusanyiko wale wanaofanya kazi ya kukamata picha. Ikiwa unawaona wakitafuta mutu wa kukamata picha, usikubali wakukamate picha.—Yoh 2:13-17.
◼ Fomu Tafadhali Fuatia Upendezi (S-43): Ukikutana na mutu yeyote anayependezwa wakati wa mukusanyiko, unapaswa kutumia fomu Tafadhali Fuatia Upendezi ili kutoa habari kumuhusu mutu huyo. Wahubiri wanapaswa kubeba fomu moja ao mbili kwenye mukusanyiko. Unaweza kuwaachia ndugu kwenye Idara ya Vitabu fomu ulizojaza ili zishugulikiwe, ao umupe mwandishi wa kutaniko lenu unaporudi nyumbani.—Soma Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 5, 2011, uku. 3.
◼ Restora: Fanya jina la Yehova liheshimiwe kupitia mwenendo wako muzuri unapokwenda kula kwenye restora. Ikiwa ni jambo la kawaida katika eneo la kwenu kumupatia mufanya kazi wa restora matabishi kidogo unaweza kufanya hivyo.
◼ Mahali Ambapo Tunapangishwa: (1) Usiwe na watu wengi zaidi katika chumba ao nyumba isivyoruhusiwa ao isivyokubaliwa na mutu aliyekukaribisha. (2) Ikiwa utavunja ombi lako la kupangishwa, fanya hivyo bila kukawia. (3) Mbele ya kupika chakula, uliza mwenye nyumba ao ndugu wanaoshugulika na upangishaji kwenye Jumba la Ufalme ili ujue kile kinachohitajiwa ili kuepuka hatari yoyote. (4) Usipitishe kiasi unapotumia vitu vyovyote vinavyotolewa kwa ajili ya wageni. Kanuni ya mwenendo ni kuwa mwenye kiasi na mwenye usawaziko. (5) Ili kumuogopa Mungu inafaa kuwa safi. Kila siku, acha mahali ulipopangishwa pakiwa na utaratibu, pakiwa safi. Hilo linahusu pia Jumba la Ufalme, ambalo linaweza kutumiwa kuwa mahali pa kupangisha ndugu waliotoka katika makutaniko ya mbali. (6) Onyesha tunda la roho unaposhugulika na wengine, iwe ni mwenye nyumba ao ndugu wengine Wakristo ambao labda munapangishwa pamoja nao—Gal. 5:22, 23.
◼ Kazi ya Kujipendea: Yeyote anayetaka kufanya kazi anapaswa kujulisha Biro ya Wafanyakazi Wanaojitolea Kufanya Kazi kwenye mukusanyiko. Watoto walio na miaka chini ya 16 wanaweza pia kusaidia kwa kutumika chini ya uongozi wa wazazi wao ao mutu aliyemuleta ao mutu mwingine mwenye kukomaa aliyekabiziwa mutoto huyo na wazazi wake.
[Sanduku katika ukurasa wa 6]
Namna ya Kumutolea Mutu Mwaliko
Ili kuwatolea watu wengi wa eneo letu mialiko, ni vizuri tusiseme mambo mengi. Tunaweza tu kusema hivi: “Jambo. Duniani pote tunajikaza kugawia watu mwaliko huu. Kamata mwaliko wako. Maelezo mengine utayasoma katika mwaliko huo.” Useme kwa uchangamfu. Unapowatolea watu mialiko Siku ya Posho ao Siku ya Yenga uwatolee pia magazeti ikiwa inawezekana.