Tutumie Kijitabu “Habari za Kujifunza Katika Neno la Mungu”—Ili Kuanzisha Mazungumuzo
1. Tumepata kifaa gani kipya kwa ajili ya mahubiri?
1 Kwenye Mukusanyiko wa Eneo wa 2014, tulipokea kijitabu chenye kichwa “Habari za Kujifunza Katika Neno la Mungu.” Namna gani tunaweza kutumia kifaa hicho kipya ili kujitayarisha kwa ajili ya mahubiri? Kwa kuwa katika kijitabu hicho, kila habari ya Biblia inategemezwa na maandiko mbalimbali, kama vile katika kitabu Kutoa Sababu, kijitabu hicho kinaweza kutusaidia sana ili kuanzisha mazungumuzo.
2. Nanma gani tunaweza kutumia kijitabu “Habari za Kujifunza Katika Neno la Mungu” katika mahubiri?
2 Unaweza kutumia ulizo la 8 na kisha kusema: “Tunatembelea watu wa eneo hili kwa dakika chache ili kujua mawazo yao juu ya ulizo hili, ‘Mungu ndiye analetea watu mateso?’ [Katika maeneo fulani, ni muzuri zaidi kumuonyesha musikilizaji ulizo hilo.] Weye unawaza nini? [Umuache ajibu.] Biblia inajibia muzuri sana ulizo hilo.” Fungua Biblia, usome na uzungumuzie andiko moja ao maandiko mengi yenye kutajwa. Kama musikilizaji anapendezwa, unaweza kumuonyesha maulizo 20 yenye kuwa mwanzoni mwa kijitabu hicho na umuombe achague ulizo moja lenye mutazungumuzia wakati utamurudilia. Ao unaweza kumutolea kichapo kimoja cha funzo chenye kuzungumuzia zaidi ulizo hilo.
3. Namna gani tunaweza kutumia kijitabu “Habari za Kujifunza Katika Neno la Mungu” ili kuanzisha mazungumuzo na watu wa dini zenye haziko za Kikristo?
3 Ulizo la 4 na maulizo ya 13 mupaka ya 17 yanaweza kusaidia zaidi sana wakati tunahubiri watu wa dini zenye haziko za Kikristo. Kwa mufano, unaweza kutumia ulizo la 17 na kusema: “Tunatembelea watu juu ya kuwatolea habari zenye zinaweza kusaidia familia. Hauone kwamba familia ziko na magumu mingi leo? [Umuache ajibu.] Shauri hili limesaidia bibi na bwana wengi: ‘Muke anapaswa kumuheshimu sana mume wake.’ [Haiko lazima kusema kwamba shauri hilo linatoka katika andiko la Waefeso 5:33. Kama unazungumuza na mwanamuke, unaweza kutaja maneno ya Waefeso 5:28.] Hauone kama shauri hilo linaweza kusaidia bibi na bwana?”
4. Wakati unamalizia mazungumuzo pamoja na mutu wa dini yenye haiko ya Kikristo, unaweza kufanya nini?
4 Wakati unamalizia mazungumuzo, upange kumurudilia musikilizaji siku ingine ili kuendelesha mazungumuzo. Unaweza kupanga kuzungumuzia andiko lingine lenye kuwa katika ulizo ambalo mulizungumuzia. Kwa wakati wenye kufaa, muambie musikilizaji kwamba mashauri mazuri yenye umemutolea yametoka katika Biblia. Umutolee kichapo fulani chenye kinaweza kumupendeza, kulingana na habari mulizungumuzia wakati uliopita na kulingana na mawazo ya mutu huyo juu ya Biblia.—Soma nyongeza ya Huduma Yetu ya Ufalme ya Mwezi wa 12, 2013.