Njia Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 3
“Watu wengi wanasherehekea kuzaliwa kwa Yesu, lakini unafikiri kwamba ni jambo la lazima kukumbuka kuzaliwa kwa Yesu?” Acha mutu ajibu. Kisha umuonyeshe Mnara wa Mlinzi wa tarehe 01/03 na musome na kuzungumuzia habari ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na musome andiko moja hivi kati ya maandiko yanayoonyeshwa. Ufanye mupango wa kumurudilia ili kuzungumuzia jibu la ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/03/12
“Leo, kuna dini nyingi, na dini hizo zina mafundisho tofauti na desturi tofauti. Unafikiri kwamba kila mutu anayejidai kuwa Mukristo ni Mukristo kwelikweli? [Acha mutu ajibu.] Kulingana na maneno ya Yesu, tazama alama moja kati ya alama zinazowatambulisha Wakristo wa kweli. [Soma Yohana 13:34, 35.] Gazeti hili linazungumuzia alama tano ambazo Yesu alionyesha ili kutusaidia tutambue ni nani walio wafuasi wake wa kweli.”
Amkeni! Mwezi wa 3
“Tunazungumuza na majirani wetu kuhusu tabia fulani yenye kuogopesha. Inaonekana kwamba watu wengi wana hasira zaidi leo na wanakasirika haraka. Unafikiri sababu ni gani? [Acha mutu ajibu.] Ona jambo fulani ambalo Biblia inasema kuhusu hasira. [Soma Zaburi 37:8.] Gazeti hili linazungumuzia sababu fulani zinazowafanya watu wawe na hasira zaidi leo na pia jinsi tunavyoweza kuzuia hasira yetu.”