Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Lugha ya Alama ya Tanzania
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • Hesabu 23
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

Hesabu—Yaliyomo

      • Maneno ya kwanza ya kishairi ya Balaamu (1-12)

      • Maneno ya pili ya kishairi ya Balaamu (13-30)

Hesabu 23:1

Marejeo

  • +Hes 22:41

Hesabu 23:2

Marejeo

  • +Hes 23:13, 14, 28-30

Hesabu 23:4

Marejeo

  • +Hes 22:20

Hesabu 23:5

Marejeo

  • +Hes 22:35

Hesabu 23:7

Marejeo

  • +Hes 23:18; 24:3
  • +Mwa 10:22; Hes 22:5; Kum 23:3, 4
  • +Hes 22:6

Hesabu 23:8

Marejeo

  • +Hes 22:12

Hesabu 23:9

Marejeo

  • +1Fa 8:53
  • +Kut 33:16

Hesabu 23:10

Marejeo

  • +Mwa 13:14, 16; 22:17; Kut 1:7

Hesabu 23:11

Marejeo

  • +Hes 24:10; Yos 24:10; Ne 13:1, 2

Hesabu 23:12

Marejeo

  • +Hes 22:38; 24:13

Hesabu 23:13

Marejeo

  • +Hes 22:11

Hesabu 23:14

Marejeo

  • +Kum 34:1
  • +Hes 22:41; 23:1, 28, 29

Hesabu 23:16

Marejeo

  • +Hes 22:35; 23:5

Hesabu 23:18

Marejeo

  • +Hes 23:7; 24:3

Hesabu 23:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “anayejuta.”

Marejeo

  • +Zb 89:35; Tit 1:2
  • +1Sa 15:29
  • +Isa 14:24; 46:10; Mik 7:20

Hesabu 23:20

Marejeo

  • +Mwa 12:1, 2; 22:15, 17; Hes 22:12
  • +Hes 22:18

Hesabu 23:21

Marejeo

  • +Kut 13:21; 23:20; 29:45; Isa 8:10

Hesabu 23:22

Marejeo

  • +Kut 20:2
  • +Hes 24:8

Hesabu 23:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Au “ubashiri.”

Marejeo

  • +Mwa 12:1, 3
  • +Hes 22:7

Hesabu 23:24

Marejeo

  • +Hes 24:9

Hesabu 23:26

Marejeo

  • +Hes 22:38; 23:12

Hesabu 23:27

Marejeo

  • +Hes 23:13

Hesabu 23:28

Maelezo ya Chini

  • *

    Au labda, “jangwa; nyika.”

Marejeo

  • +Hes 21:20

Hesabu 23:29

Marejeo

  • +Hes 22:41; 23:1, 14

Jumla

Hes. 23:1Hes 22:41
Hes. 23:2Hes 23:13, 14, 28-30
Hes. 23:4Hes 22:20
Hes. 23:5Hes 22:35
Hes. 23:7Hes 23:18; 24:3
Hes. 23:7Mwa 10:22; Hes 22:5; Kum 23:3, 4
Hes. 23:7Hes 22:6
Hes. 23:8Hes 22:12
Hes. 23:91Fa 8:53
Hes. 23:9Kut 33:16
Hes. 23:10Mwa 13:14, 16; 22:17; Kut 1:7
Hes. 23:11Hes 24:10; Yos 24:10; Ne 13:1, 2
Hes. 23:12Hes 22:38; 24:13
Hes. 23:13Hes 22:11
Hes. 23:14Kum 34:1
Hes. 23:14Hes 22:41; 23:1, 28, 29
Hes. 23:16Hes 22:35; 23:5
Hes. 23:18Hes 23:7; 24:3
Hes. 23:19Zb 89:35; Tit 1:2
Hes. 23:191Sa 15:29
Hes. 23:19Isa 14:24; 46:10; Mik 7:20
Hes. 23:20Mwa 12:1, 2; 22:15, 17; Hes 22:12
Hes. 23:20Hes 22:18
Hes. 23:21Kut 13:21; 23:20; 29:45; Isa 8:10
Hes. 23:22Kut 20:2
Hes. 23:22Hes 24:8
Hes. 23:23Mwa 12:1, 3
Hes. 23:23Hes 22:7
Hes. 23:24Hes 24:9
Hes. 23:26Hes 22:38; 23:12
Hes. 23:27Hes 23:13
Hes. 23:28Hes 21:20
Hes. 23:29Hes 22:41; 23:1, 14
  • Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
Tafsiri ya Ulimwegu Mpya
Hesabu 23:1-30

Hesabu

23 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Jenga madhabahu saba mahali hapa,+ nawe unitayarishie ng’ombe dume saba na kondoo dume saba.” 2 Mara moja Balaki akafanya kama Balaamu alivyomwambia. Kisha Balaki na Balaamu wakatoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 3 Halafu Balaamu akamwambia Balaki: “Kaa hapa karibu na dhabihu yako ya kuteketezwa, nami nitaenda. Labda Yehova atawasiliana nami. Jambo lolote atakalonifunulia, nitakwambia.” Basi akaenda juu ya kilima kilicho wazi.

4 Ndipo Mungu akawasiliana na Balaamu,+ Balaamu akamwambia: “Nilijenga safu za madhabahu saba na kutoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.” 5 Yehova akatia maneno haya katika kinywa cha Balaamu:+ “Rudi kwa Balaki, na hili ndilo utakalosema.” 6 Basi akarudi na kumkuta Balaki na wakuu wote wa Moabu wakiwa wamesimama karibu na dhabihu yake ya kuteketezwa. 7 Kisha akasema maneno haya ya kishairi:+

“Balaki mfalme wa Moabu amenileta kutoka Aramu,+

Kutoka katika milima ya mashariki:

‘Njoo umlaani Yakobo kwa niaba yangu.

Naam, njoo uwashutumu Waisraeli.’+

 8 Ninawezaje kuwalaani watu ambao Mungu hajawalaani?

Ninawezaje kuwashutumu wale ambao Yehova hajawashutumu?+

 9 Kutoka juu ya miamba ninawaona,

Na kutoka vilimani ninawatazama.

Wanaishi peke yao kama taifa;+

Hawajioni kuwa sawa na mataifa mengine.+

10 Ni nani anayeweza kuhesabu chembe za mavumbi ya Yakobo+

Au hata kuhesabu robo ya Waisraeli?

Acha nife kifo cha watu wanyoofu,

Na mwisho wangu uwe kama wao.”

11 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Kwa nini umenitendea hivi? Nilikuleta ili uwalaani maadui wangu, lakini badala yake umewabariki tu.”+ 12 Balaamu akasema: “Je, sipaswi kusema neno lolote ambalo Yehova anatia kinywani mwangu?”+

13 Balaki akamwambia: “Tafadhali, twende mahali pengine ambapo unaweza kuwaona. Utaona baadhi yao; hutawaona wote. Ukiwa huko walaani kwa niaba yangu.”+ 14 Kwa hiyo akampeleka kwenye uwanja wa Sofimu, juu ya Pisga,+ naye akajenga madhabahu saba na kutoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.+ 15 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Kaa hapa karibu na dhabihu yako ya kuteketezwa ninapoenda pale kuwasiliana Naye.” 16 Basi Yehova akawasiliana na Balaamu na kutia neno hili kinywani mwake:+ “Rudi kwa Balaki, na hili ndilo utakalosema.” 17 Basi akarudi na kumkuta Balaki akisubiri karibu na dhabihu yake ya kuteketezwa, na wakuu wa Moabu walikuwa pamoja naye. Balaki akamuuliza: “Yehova amesema nini?” 18 Kisha Balaamu akasema maneno haya ya kishairi:+

“Inuka, Balaki, usikilize.

Nisikilize, ewe mwana wa Sipori.

19 Mungu si mwanadamu anayesema uwongo,+

Wala si binadamu anayebadili nia yake.*+

Akisema jambo, je, hatalitenda?

Akinena jambo, je, hatalitimiza?+

20 Tazama! Nimeletwa ili nibariki;

Sasa Yeye amebariki,+ nami siwezi kubadili.+

21 Havumilii nguvu zozote za uchawi dhidi ya Yakobo,

Wala haruhusu taabu yoyote impate Israeli.

Yehova Mungu wake yuko pamoja nao,+

Nao humsifu kwa sauti kubwa kuwa mfalme wao.

22 Mungu anawatoa Misri.+

Yeye ni kama pembe za fahali mwitu.+

23 Kwa maana hakuna ishara za msiba dhidi ya Yakobo,+

Wala hakuna uaguzi* wowote dhidi ya Israeli.+

Sasa inaweza kusemwa hivi kumhusu Yakobo na Israeli:

‘Tazameni mambo ambayo Mungu ametenda!’

24 Watu hawa watainuka kama simba,

Na kama simba, watajiinua.+

Hawatalala chini mpaka wale mawindo

Na kunywa damu ya waliouawa.”

25 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Ikiwa huwezi kamwe kuwalaani, basi usiwabariki pia.” 26 Balaamu akamwambia Balaki: “Je, sikukwambia, ‘Nitafanya mambo yote ambayo Yehova anasema’?”+

27 Ndipo Balaki akamwambia Balaamu: “Tafadhali njoo nikupeleke mahali pengine. Labda Mungu wa kweli atakubali uwalaani kwa niaba yangu kutoka mahali hapo.”+ 28 Basi Balaki akampeleka Balaamu juu ya Mlima Peori, unaoelekeana na Yeshimoni.*+ 29 Kisha Balaamu akamwambia Balaki: “Jenga madhabahu saba mahali hapa, nawe unitayarishie ng’ombe dume saba na kondoo dume saba.”+ 30 Kwa hiyo Balaki akafanya kama Balaamu alivyomwambia, naye akatoa dhabihu ya ng’ombe dume mmoja na kondoo dume mmoja juu ya kila madhabahu.

Tanzanian sign language publications(2020-2025)
Toka
Ingia
  • Lugha ya Alama ya Tanzania
  • Shiriki
  • Mapendezi
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Masharti ya Utumiaji
  • Sera ya Faragha
  • Mpangilio wa Faragha
  • JW.ORG
  • Ingia
Shiriki